(Vatican Radio) Baba Mtakatifu Francisko wiki hii alitoa nyaraka mbili za “Motu proprio”zinazolenga kufanya mabadiliko katika Mfumo wa Mahakama ya Kanisa Katoliki juu ya uendeshaji wa kesi zinazohusiana na sheria ya ndoa.
Papa alitoa nyaraka hizo siku ya Jumanne, Motu proprio, “Mitis Iudex Dominus Jesus”au
Bwana Yesu, Hakimu mwenye huruma", ambayo inarekebisha kanuni za mahakama ya sheria
ya kanisa (CIC) kwa Makanisa ya Amerika, na barua nyingine, “mitis et misericors Jesus"Msamaha
na huruma ya Yesu”, ambayo inafanya inarekebisha Kanuni za Makanisa za Kanisa katika
uendeshaji wa kesi za kubatilisha ndoa kwa Makanisa ya Mashariki (CCEO).
Profesa katika Sheria za Kanisa katika Chuo Kikuu cha Kipapa ya Gregorian Rome, Padre
James Conn, SJ, akizungumzia marekebisho hayo ameiambia Redio Vatican kwamba, kuna
mabadiliko maalum matatu , hasa katika uharakisha wa kushughulikia kesi za wanaondoa
wanaotaka kubatilisha ndoa; kuondolewa kwa haja ya mahakama kutoa hukumu mara mbili
kwa tukio na kisha tena kupelekwa katika mahakama ya rufaa, kwa maana kwamba, inatosha
kuzingatia maamuzi yaliyotolewa na mahakama kwa mara ya kwanza, iwapo yanayoona kwamba
, kuna ushahidi wa kutosha kwa ndoa kutanguliwa, na wahusika wanaweza kufunga ndoa
ndoa mpya kwa mujibu wa sheria Kanisa (au katika kupokea miungano ya ndoa ilifungwa
kwa sheria za kiraia , wakati huo huo kutambuliwa na Kanisa).
Pia kuanzishwa kwa uwezekano wa kesi kusikilizwa na hakimu mwenye uzoefu mara
moja, kama hatua ya kupunguza mzigo wa wingi wa kesi katika mahakama za majimbo, ambako
watu wenye ujuzi ni wachache); Na uundaji wa kueleka mchakato wa kesi katika baadhi
ya kesi , kutolewa maamuzi moja kwa moja na Askofu mahalia, kwa kesi ambazo zina ushahidi
wa kutosha kutolewa hukumu ya kubatishwa na pande zote mbili zinaamini muungano wao
ulikuwa batili. Katika mchakato huu hasa unaonyesha dhamira Papa Francisco kugawana
madaraka na Maaskofu wa majimbo duniani kote.
Prof Conn, SJ, aliendelea kufafanua kwamba - kinyume na uvumi uliotolewa na baadhi
ya vyombo vya hata katika vyombo vya Kanisa, mabadiliko yamefanyika katika misingi
ya uelewa wa Kanisa la asili na muundo wa kimsingi wa ndoa, na hivyo hakuna mabadiliko
kaika Madhumuni msingi na katika wigo wa mfumo wa Mahakama wa Kanisa. Na wala hakuna
mabadiliko katika mafundisho ya Kanisa juu ya kutengua ndoa, alisema Prof. Conn,
SJ. Na kwamba, nyaraka mpya za mabadiliko hazibadilishi kanuni zinazofuatwa na Mahakimu
katika kubatilisha ndoa na wala hazibadili uhalali wa ndoa, hivyo, ndoa kubatilishwa
linabaki ni jambo linalohitaji uwepo wa ushahidi wa kutosha .
All the contents on this site are copyrighted ©. |