2015-08-29 12:55:00

Józef Wesolowski amefariki kawaida


Uchunguzi wa  mwili wa Askofu Józef Wesolowski, umekamilika na matokeo kwamba amekufa kifo cha kawaida. 

Kufuatia kifo cha ghafla, kilichotokea Alhamisi Augosti 27 ndani nyumba ya Vatican,  kwa Joseph Wesolowski , aliyekuwa Mjumbe wa  Kitume huko San Domenico,  Ofisi ya utetezi wa   Sheria Vatican, kama sehemu ya majukumu ya mamlaka ya sheria Vatican, imetangaza kwamba , Marehemu  Josef Wesolowski  amefariki kwa kifo cha kawaida.  Maelezo haya yametolewa baada ya kutekelezwa agizo la mwili wa marehemu uchunguzwe kitalaam kujua chanzo au asili ya kifo hicho. Na hivyo Mamlaka ya sheria iliteua Tume maalum ya wataalamu tatu, chini ya uratibu na Prof John Arcudi, Profesa wa uchunguzi wa kidaktari katika Chuo Kikuu cha Rome "Tor Vergata".

Uchunguzi ulifanyika  siku ya Ijumaa alasiri matokeo yake yamethibitisha  kwamba ni kifo cha kawaida, kilichotokana na mapigo ya moyo kusimamisha. Mara kilipotokea kifo hiki, Ofisi ya utetezi wa Sheria, ilitaka kupata  matokeo ya vipimo vya uchunguzi wa maabara uliofanywa na Tume hiyo.

Marehemu  Józef Wesolowski  alizaliwa Julai 15, 1948 Poland. Baada ya kukamilisha masomo yake ya kikuhani, alilitumikia Kanisa katika ngazi mbalimbali, na mwaka 2008 aliteuliwa na Papa Bendikto XVI,  kuwa Mjumbe wa Kitume wa Papa katika Jamhuri ya Kisiwa cha Domenicani hadi Agosti 13, 2013, alipoachishwa kazi hiyo na Vatican kufuatia tuhuma za kudhulumu watoto kinjisia. Mwaka 2014, alivuliwa cheo cha Askofu Mkuu na kinga ya kidiplomasia ili  Mamlaka katika Jamhuri ya Domenicani iweze kuchunguza madai ya unyanyasaji wa watoto yaliyotolewa  dhidi yake. Hivyo vyombo vya kisheria vya Vatican vilikuwa bado vikifuatilia kesi yake. 








All the contents on this site are copyrighted ©.