2015-08-20 10:38:00

Mashariki ya kati bado usalama si shwari


Hali ya usalama na amani Mashariki ya Kati bado ni ndoto ya kufikirika. Taarifa zinabaini katika kipindi cha saa 24 kwa Jumatano iliyopita, kulikuwa na mwendelezo wa mashambulio ya kushtukiza, vurugu na mashambulizi ya kutumia mabomu katika maeneo kadhaa nchini Uturuki, Misri, Syria na Iraq, kati ya  magaidi na  vikosi vya usalama serikali. Aidha utamaduni wa kukata vichwa mateka bado unafanywa na kikosi cha Kiislamu cha ISIS,ambacho kimefanya mauaji ya aina hiyo kwa Mtalaam wa mambo ya kale ya Palmyra, Mkongwe mwenye miaka 82.

Marco Guerra anaendelea kuripoti kwamba, gari lenye bomu lililotegeshwa lililipuka  karibuni katika wakati wa vurugu za chaguzi Mashariki ya Kati, na kujeruhi watu 24,  shambulio lililofanyika  mbele ya makao makuu ya vikosi vya usalama nje kidogo ya Kaskazini mwa  mji Mkuu wa Cairo. Mashambulizi yanayodaiwa kufanywa na Chama kinachojiita “Egypt  Black  Block”.

Aidha wasiwasi na hofu zimetawala katikati ya mji wa  Istanbul, ambako Jumatano nyakati za  alasiri ya milio ya risasi  ilisikika  nje ya  eneo maarufu la Ikulu “Dolmabahce”ambayo pia ni  makao makuu ya ofisi mwakilishi wa waziri mkuu wa Uturuki. Watu wawili waliokamatwa na polisi kuhusika na shambulio hilo wametajwa kuwa ni kutoka kikundi cha uhalifu cha Mlengo wa kushoto. Aidha chama cha PKK kinahusishwa na shambulio lililoua askari wanane nane  mjini  Ankara.

Na huko Syria, katika mapambano kati ya majeshi Wakurdi na wapinganaji wa Kiislamu wa IS , yalisababisha magaidi 13 kupoteza maisha. Jambo lililokasirisha wanamgambo wa Isis, na kutekeleza adhabu ya kumkata kichwa aliyekuwa Mtalaam katika mambo ya kale ya Asaad, mwenye umri wa miaka 82,  Mtaalam na mkurugenzi wa mambo ya kale  katika tovuti ya Palmyra ya zamani.

Aidha hali si shwari huko Iraq ambako taarifa zinataja uwepo wa majeruhi 20, kutokana na mabomu ya kujiua yaliyolipuka kama  kuendelea uvamizi wa Shirikisho la wapiganaji wa Kiislamu, wasiovumilia wengine.

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.