Kipindi cha mapumziko baada ya kazi, ni zawadi ya thamani ambayo Mungu alifanya
kwa familia ya binadamu", ambayo haipaswi kupita au kupuuzwa katika mipango ya utendaji
wa familia na mtu binafsi . Ni maelezo ya Papa aliyoyatoa siku ya Jumatano wakati
wa katekesi yake kwa mahujaji na wageni waliokuwa wamekusanyika katika Ukumbi wa Paulo
VI,mjini Vatican. Papa Francisko alitoa wito kwa familia kuiishi kama inavyotakiwa
Siku ya Mapumziko ya Jumapili, kwa kushiriki katika Ibada ya Ekaristi inayobadili
kila wakati wa maisha, hata wakati wa uchungu. Katika Katekesi hii, Papa aliwakumbatia
wakimbizi Wakristo kumi waliowasili tokea kituo cha Wakimbizi cha Lampedusa Italia
baada ya kutoroka vurugu nchini Nigeria na kuuishi miezi sita ya kazi ya kulazimishwa
nchini Libya.
Papa akitafakari umuhimu wa mapumziko ya baada yakazi, alisema, mapumziko yaliwekwa
na Mungu mwenyewe,kama nafasi ya kutafakari uzuri wa kile kilichofanyika au kuumbwa
kama Mwenyezi Mungu mwenyewe alivyofanya baada ya kuiumba dunia na vyote vilivyomo.
Na hivyo mapumziko inakuwa nafasi nyingi wazi ya kufikiria pia jinsi ya kusonga
mbele kwa mafanikio zaidi katika kazi.
Papa alieleza kwa kuangalisha katika kitambu cha Mwanzo, aya zinazozungumzia jinsi
Mungu alivyoumba dunia na vilivyomo vyot, na jinsi baada ya kuviumba vyote alipata
siku ya kupumzika y akutafakari yote yaliyofanyika. Hivyo siku mapumziko ilibuniwa
na Mungu mwenyewe na akaibariki na kuitakatifusha. Kwa hiyo mwanzo wa kuwa na mapumziko
ni upendo na hamu ya Mungu. Papa Francisko aliendelea kukumbusha umati wa watu, kwamba,
kubarikiwa kwa siku ya saba kunatufundisha umuhimu wa kuwa na muda wa kutafakari na
kufurahia kazi zile zilizofanyika katika muda wa siku sita za wiki.Na si tu katika
maana ya kitaaluma lakini pia kwa maana ya kila utendaji wa wanaume na wanawake hata
katika maisha ya familia, kwa namna nyingine inaweza kusemeka kuwa jinsi tulivyoshirikishana
katika kazi ya ubunifu wa Mungu.
Kwa hiyo kupumzika si kama uvivu au kujibweteka, lakini ni wakati mzuri wa kutazama
kwanza ya yote yaliyofanyika kwa upendo na kutathimini kazi kwa makini zaidi. Na ndivyo
ilivyo hata kw amaisha ya familia , ya bibi na bwana harusi,baada ya kazi kubwa walizozifanya
wakati wa uchumba, hufunga ndoa na kuingia katika kipindi cha mapumziko, kipindi cha
kutafakari maisha yao mapya, hii ni jambo jema. Kwa wazazi baba na mama, mapunziko
ni muda wa kuangalia watoto au wajukuujinsi wanavyokua na jinsi ya kuunda mfumo wao
wa maisha ya baadaye. Kipindi chamapumziko ni wakati wa kutazama kwa makini yanayotakiwa
kufanyika ndani ya nyumba zetu, katika kujenga urafiki zaidi na wengine na jamii
inayotuzunguka, na kufikiria juu ya mazuri zaidi.
Aidha Papa alionyesha kusikitika kwamba , bahati mbaya kumejengeka tabia na mwelekeo wa matumizi mabaya ya siku ya Mapumziko. Wengi huitumia kama siku ya kufuja maisha na mali, wakiyaweka maisha hatarini. Badala ya kuwa katika hali za utulivu wa kutafakari kazi za siku sita, siku ya mapumziko inakuwa ni siku yenye vurugu zaidi kijamii.Wengine wakitafuta kujineemesha zaidi na siku ya mapumziko iliyowekwa na Mungu. Siku ya mapumziko, hasa zaidi Jumapili ni siku iliyowekwa kwa ajili ya tafakari na si ya kufanya tena kazi za uzalishaji mali.
Baba Mtakatifu Francisko, alileleza hili katika mwendelezo wa mada juu ya Familia , akiwataka wote waliokuwa wakimsikiliza kutafakari pamoja nae mambo makuu matatuyasiyoweza kwepeka katika maisha ya familia nayo ni :Mapumziko, Kazi na Sala.
Na mwisho wa katekesi yake alisalimia mahujaji na wageni kwa lugha mbalimbali, akiwataja wanaozumguza lugha ya Kiingerezahasa kutoka Malta, Zimbabwe, Philippines na Trinidad na Tobago. Aliwatakia wote baraka zake za kitume na huruma ya Bwana.
All the contents on this site are copyrighted ©. |