2015-08-11 12:49:00

Papa ataja Siku ya Dunia ya kuombea viumbe


Baba Mtakatifu Francisko ameitaja kwa mara ya kwanza, Tarehe Mosi Septemba ya  kila mwaka iwe ni Siku ya Dunia ya kuombea viumbe na ekolojia. Katika kuitaja Siku hii, amehimiza Wakristo wote duniani kutoa angalisho makini katika utunzaji wa viumbe na asili, akisema ni wajibu unaokwenda sambamba na uongofu  wa kiroho.  Papa ameeleza hilo katika barua yake aliyowatumia Makardinali Peter Turkson Rais wa Baraza la Kipapa  kwa ajili ya Haki na Amani na Kardinali Kurt Koch Rasi wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Umoja wa Wakristo. Imeelezwa  Papa amewatumia viongozi hao kutokana na Siku hii  ya kujali viumbe na asili kuwa na tabia  ya kiekumeni, na pia ni siku ambayo tayari huadhimishwa na Kanisa la Kiotodosi.

Kutangazwa kwa Siku hii, inatajwa kuwa ni matokeo ya Waraka wa Papa Francisko wa hivi karibuni wa “Laudato Si” “Sifa kwako juu ya utunzaji wa dunia Nyumba ya wote, ambamo Papa Francisco , ameonyesha hamu yake  kwamba, iwepo siku  katika mtazamo wa kuekumeni, Wakristo kwa pamoja, kutoa maombi, sala, na agalisho makini kwa ajili ya huduma kwa viumbe. Papa katika waraka wake pia nukuuu  kwa michango iliyotolewa na Patriaki  Bartholomayo I, na  Askofu Mkuu Ioannis.  Kwa maana hiyo  basi,  Siku ya kuombea viumbe basi inaweza tajwa kuwa  asili yake ni   waraka  huo wa Laudato Si..

Papa Francisko, katika barua yake kwa Makardinali anarudia kuhimiza kwamba, uongofu wa Mkristo huenda sambamba  na tabia njema  za kushughulikia viumbe na mazingira kwa hekima, busara na unyenyekevu, wenye kulishwa na urithi wa utajiri kiroho wa Kikristo. Na hiyo inamaana kubwa na muhimu kwa Wakristo, katika utoaji wa mchango wao,  kwa ajili ya kuvishinda vipeo  na changamoto dhidi ya  mazingira, vinavyokabili ubinadamu leo hii.

Barua inaendelea kukumbusha kwamba, maisha ya kiroho hayawezi kutenganishwa na asili, lakini vyote viwili hutembea pamoja katika  umoja.  Hivyo, ameonya, uogofu wa kweli, ni pamoja na kujali mazingira asili ya ekolojia, kwa kuwa mazingira ni kazi ya Mungu,  aliyokabidhiwa binadamu kuilinda na kuitunza kama sehemu muhimu ya maisha adilifu ya Mkristo.

Papa aliendelea kutoa  wito kwa Wakristo, kuomba msahama na huruma ya Mungu kwa dhambi zinazofanywa na binadamu dhidi ya viumbe na asili. Kwa  mtazamo huu anasema, Siku ya  Maombi kwa ajili ya viumbe na asili, inakuwa ni  nafasi  ya kipekee, kwa  waumini na jamii, kwa ajili ya kufanya upya ahadi zao katika wito wa kuwa mawakili wa viumbe, na kumshukuru Mungu  kwa "kazi yake ya  ajabu" waliokabidhiwa  binadamu na zaidi sana kwa ajili ya kuomba huruma yake , kwa ajili ya dhambi tunazofanya dhidi ya mazingira na ekolojia ya dunia tunamoishi.

Wakatoliki na Waotodosi, kuwa na maombi kwa nia moja ya kuombea viumbe, inakuwa ni fursa ya kushuhudia kukua kwa ushirikiano miongoni mwa Wakristo. Kwa hiyo , Papa ametoa msisitizo kwa Wakristo kuitikia wito huu kwa uaminifu na ufanisi zaidi, kwa ajili ya kukabiliana na changamoto dhidi ya mazingira na katika kutoa jibu la pamoja muhimu katika kujenga matumaini, amani  na  ustawi katika vyote kihali na kiroho kwa watu wote.  sasa na hata kwa siku za baadaye.  Papa ameomba pia kuhusisha makanisa mengine sambamba na mipango iliyokwisha pendekezwa na kufanikishwa na Baraza la Makanisa la Dunia. .

Barua ya Papa kwa Makardinali Peter Turkson na Kurt Koch, imehitimu kwa  kuomba msaada wa Bikira  Maria,  Mama wa Mungu, na kwa Mtakatifu Francis wa Asisi,  na  Wimbo wa Masifu juu ya viumbe , wenye kuvuvia wake kwa waume wengi wenye mapenzi mema, kuishi kwa kumtukuza Muumba wa Viumbe na katika kuheshimu viumbe Na pia kama ilivyokwisha pendekezwa na Baraza la Maaskofu Katoliki la Italia,  katika mkutano wake wa kumi wa mwaka huuuliofanyika  chini ya Mada mbiu : ubinadamu mpya kwa ajili ya maisha duniani.

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.