Baba Mtakatifu Francisko, amepeleka ujumbe wa mshikamano kwa wakimbizi, ambamo kwa nguvu pia anaihimiza jumuiya ya kimataifa, kukabiliana kwa nguvu zote na vipeo vya uhalifu wa haki za binadamu unao endelea Mashariki ya Kati.
Baba Mtakatifu ametuma barua hiyo kwa Askofu Mkuu Maroun Lahham wa Jerusalem ambaye
pia ni Vika wa Yordani , akionyesha mshikamano wake kwa mamia ya maelfu ya wakimbizi
wa Iraki wanaoishi Yordani waliokimbia madhulumu na mauaji akiwataja kuwa ni wafia
dini wa leo.
Kwa mwaliko wa Askofu Mkuu Lahmam na Patriaki wa Jerusalme Mashariki. Askofu Mkuu Fouwad Toual, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu la Italia, Askofu Mkuu Nunzio Galantino, kwa wakati huu anatembelea Yordan, kwa lengo la kushiriki katika kumbukumbu ya kupita mwaka mmoja tangu kuwasili kwa wakimbizi wa Iraki nchini Yordani. Katika tukio hili, Askofu Mkuu Galantino, atashiriki katika matukio mbalimbali yaliyoandaliwa kwa ajili ya kumbukumbu hii.
Ujumbe Baba Mtakatifu kwa wakimbizi wa Yordani , umeanza na maneno ya kuwatia matumaini
ndugu hawa walioonewa na kuziishi hali za vurugu hadi kulazimika kuachana na nyumba
zao na nchi yao.
Papa pia amekemea vikali uwepo wa dhuluma mateso na mauaji ya kinyama yasioweza elezeka
yanayofanya na watu wasiovumilia wengine, ushabiki unaoathiri , ambao haiwezekani
kunyamaliwa au kupuuzwa au kukaliwa kimya na jumuiya ya kimataifa.
Papa amewataja watu hao wanaonewa na kuuawa kwa sababu ya imani yao , kuwa ni mashahidi
wafia dini wa leo, wanyonge na wanaobaguliwa kwa sababu ya uaminifu wao kwa Injili.
Aliendelea kukumbusha jinsi Kanisa lisivyo weza kusahau au kuwatelekeza wafuasi wake,
hata wale walio uhamishoni kwa sababu ya imani yao. Papa amewashukuru wakimbizi wote
kwa uthabiti wa imani na ushahidi wao.
Papa pia katika ujumbe wake hakusahau kuwataja wale wanaosaidia mamia ya maelfu ya
wakimbizi akisema, utumishi wao unatangaza ufufuo wa Kristo," na msaada wa ni mwanga
wa matumaini wakati wa uwepo wa giza. Amewaombea wingi wa baraka za Bwana maana
ndiye mtoaji pekee wa zawadi nyingi .
Ujumbe wa Papa , umeonyesha hamu yake ya kuona duniani nzima inajali kwa makini na
kwa kina zaidi, mateso ya watu hao na hivyo kuwa tayari kushiriki katika hatua zote
za kukomesha uso wa mateso yanayofanyika, na kushikamana na Wakristo na jumuiya zingine
za kidini hasa zenye waumini wachache wanaodhulumu haki yao ya kuishi kwa uhuru na
amani .
Papa kwa mara nyingine, ametoa ombi lake kwa Jumuiya ya Kimataifa, akiitaka isikae
kimya mbele ya jinamizi hili la uso wa uhalifu usiokubalika, au kupuuzwa maana ni
kitisho kwa haki za binadamu na huzuia utajiri wa mshikamano kati ya watu, tamaduni
na dini.
Papa Francis alihitimisha kwa kuomba sala na maombi kwa ajili yao , na kuwapa Baraka
zake za Kitume na kuwakabidhi chini ya ulinzi wa kimama a Bikira Maria.
All the contents on this site are copyrighted ©. |