(Vatican Radio) Papa Francisko Jumanne majira ya jioni, alikutana na maelfu ya vijana watumishi wa altareni , kutoka mataifa mbalimbali ya Ulaya, waliokusanyika katika Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro hapa Vatican. Hii ilikuwa ni sehemu ya tisa ya hija ya Kimataifa ya vijana watumishi wa altareni kutembelea Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro.
Katika hotuba yake Papa Francisko alitafakari juu ya madambiu ya hija ya mwaka huu, "Mimi hapa! Nitumie". Baba Mtakatifu aliwaambia vijana, "Ni muhimu kutambua kwamba, kuwa karibu na Yesu na kujua uwepo wake katika Ekaristi kwa njia ya huduma yao altareni, huwawezesha wao kujifunua wenyewe kwa wengine,na kusafiri pamoja katika ufanikishaji wa malengo muhimu pamoja, na katika kupata nguvu ya kufanikisha malengo hayo.
Hija Kimataifa ya Watumishi wa Altareni, hufanyika kila baada ya miaka mitano,
na huandaliwa na chama cha Kimataifa cha watumishi a Altareni cha “Coetus Internationalis
Ministrantium”, pamoja na wawakilishi kutoka nchi kadhaa za Ulaya, ikiwa ni pamoja
na Ujerumani, Italia, na Ufaransa, Croatia, Luxembourg, Serbia, na Slovakia. Hija
hii ya kimataifa ya watumishi altareni hulenga kuwapa washiriki uzoefu wa kipekee,
kwa ajili ya huduma yao altareni na kama msaada katika kugundua yaliyomo katika huduma
za Kanisa la Ulimwengu .
Baba Mtakatifu Francisko katika hotuba yake, aliwashukuru kwa moyo wa dhati wote walioshiriki
katika hija hii maelfu ya vijana baadhi yao wakiwa wamesindikizwa na wazazi au walezi
wao, bila kujali joto kali la mwezi Agosti hapa Roma. Na alitoa shukurani za pekee
kwa Askofu Nemet, Rais wa juhudi hizi , kwa maneno yake ya mazuri ya utangulizi na
salamu. Na kwa ajili ya hija hii katika mji wa Roma, mji ambapo Mitume Petro na Paulo
walikuwa mashahidi.
Papa aliendelea kusema, ni muhimu kwao kutambua kwamba, kuwa karibu na Yesu na kumjua
katika Ekaristi kwa njia ya huduma yao altareni, kutawawezesha wao kujifunua wenyewe
kwa wengine, katika kusafiri pamoja, kulenga pamoja na katika kupata nguvu za kufanikisha
malengo yao. Papa alieleza, “ni mwanzo wa kuwa na furaha ya kweli kutokana na kutambua
kwamba, licha ya kuwa wadogo na dhaifu, kwa msaada wa Yesu, wanaweza kuwa na nguvu
za kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika safari kubwa ya maisha yao kwa
kuwa pamoja na Yesu.
Papa alieleza na kuwahimiza wote waliokuwa wakimsikiliza kuwa kama Nabii Isaya,
alivyogundua ukweli huu na kumwomba Mungu aitakase nia yake, kumsamehe dhambi zake,
kuiponya roho yake, kumfanya tayari kuchukua kazi muhimu ya kupeleka Neno la Mungu
kwa watu wake. Katika kufanya hivyo, akawa chombo cha uwepo wa huruma ya Mungu miongoni
mwa watu. Isaya alitambua kwamba, kwa kujikabidhi mwenyewe katika mikono ya Bwana,
Maisha yake yote yatabadilika. Papa alieleza na kuongeza kwa jinsi ilivyo vizuri kutambua
kwamba, imani humwenzesha mtu mwenyewe kujitambua alivyo na kumtoa nje ya kujitenga,
kwa sababu hujawa na furaha ya kweli ya katika urafiki na Yesu Kristo. Imani humuunganisha
mtu kwa wengine na kumfanya kuwa mmisionari asili!
Papa alieleza na kuwakaribishana vijana na kutoa mwaliko kwao wote watumishi wa altareni,
wavulana na wasichana ,akiwataka zaidi ya yote , wakumbuke kuzungumza na Yesu katika
maombi yao ya kila siku; zaidi wakijilisha na Neno la Mungu na Mwili wa Bwana, kama
silaha na njia bora zaidi ya kupata nguvu za kutoka nje, kwenda kukutana na wengine,
kuwapelekea zawadi waliyoipokea kutoka kwa Bwana wanayemtumikia, na kuitoa kwa wengine
kwa shauku ya furaha waliyopokea.
Papa alikamilisha hotuba yake kwa kuwashukuru wote kwa kutumikia altare ya Bwana na
kwa ajili ya kuifanya huduma hii, kuwa shule halisi ya kujifunza imani, na upendo
kwa jirani. Na pia aliwashukuru kwa kuanza kuitikia wito wa Bwana kama ilivyokuwa
kwa Nabii Isaya , kusema "Mimi hapa. Nitumie "(Isa 6: 8).
All the contents on this site are copyrighted ©. |