2015-07-21 09:21:00

Watu saba watekwa nyara Libya wakiwemo wakristo watatu


Nchini Libya , watu saba walitekwa nyara siku ya Jumapili , wakiwa ni Wakristo watatu,  raia wa Ghana, Nigeria na Misri, na Waitaliani wanne. Habari inasema, wanne ni mafundi  waajiri wa Kamupuni ya kujitegemea ya  Bonatti, inayo husika na  malipo ya wahandisi, wajenzi na wasimamizi katika sekta ya  matengenezo ya  nishati.

Utekaji nyara huo ulifanyika katika Kikuu cha gesi katika Mji wa Mellitah  ambao ni Makao Makuu ya Mtambo wa gesi asilia Libya, na ni sehemu ya  mtandao wa bomba kubwa la gesi linalopita chini ya bahari lenye urefu wa km 520, lililolazwa katika kina cha zaidi ya 1,100 mita kwenda chini , hadi katika kituo chake cha mwisho cha  Gela,  Sicily Italy. Bomba hilo hutoa gesi ya ujazo wa mita bilioni 10 za gesi kwa mwaka kwa  ajili ya bara la Ulaya. .

Kwa  mujibu wa televisheni Kiarabu Al Jazeera, kati ya waliotekwa Jumapili, wanne walikuwa walitekwa karibu na eneo linalojulikana kuwa makazi ya  Jeshi la kikabila, wanamgambo wanaomuunga mkono jenerali  Haftar anayeongoza  serikali ya Tobruk ambacho ni kikundi cha mapambazuko ya kisiasa ya Tripoli  Libya.  Juu ya utekaji nyara huu,  ubalozi wa Libya kwa Kitakatifu, umeingilia kati akisema kuwa, tendo hilo lina lenga kuishinikiza Italy kutoa mchango wake  katika mazungumzo ya amani juu ya mgogoro wa Libya.

Na waafrika watatu wametekwa nyara na kundi kinachohisiwa kuwa wanachama wa serikali ya wapiganaji wa kidini wa Kiislamu wa Daesh.  Tetesi  za watu  hao kutekwa nyara, zilivuma tangu tarehe  11 Julai, lakini zimethibitishwa siku ya Jumapili iliyopita na msemaji wa kijeshi wa serikali ya Libya, ambao kwa sasa imeweka makao yake makuu  Tobruk ikitambuliwa na jumuiya ya kimataifa

Kundi jihadi limedai kuhusika na utekaji nyara, kwa kutoa tamko hilo kwenye vyombo vya habari vya jamii na kuweka picha za vitambulisho vya mateka watatu, bila kutoa maelezo zaidi. Kwa mujibu wa vyanzo Misri waliohojiwa na Fides, juhudi za kuwaokoa mateka zinafanyika pengine ikilazimu kulipa fidia.

Kutokana na hali ngumu ya usalama nchini Libya, Wizara ya Nje mambo ya Nje , kwa muda mrefu imekuwa ikishauri  wananchi na wageni  kwenda nchi za Kaskazini mwa Afrika kwa madhumuni ya kazi tu. Waziri Gentiloni, anasema kwamba, upinzani bado mkali hivyo ni vigumu kubashiri vitendo vya kigaidi na utekaji nyara. 








All the contents on this site are copyrighted ©.