2015-07-10 09:10:00

Hotuba ya Papa kwa Wanakanisa -Ninyi ni mashahidi wa upendo na huruma ya Yesu


Baba Mtakatifu Francisko akiwa katika ziara yake ya Kitume nchini Bolivia, Alhamisi , baada ya kuongoza Ibada ya mIsa asubuhi katika uwanja wa La Paz, majira ya jioni alikuwa na mikutano miwili. Kwanza Mkutano na Watumishi wa Kanisa, Mapadre, Watawa wa kike na Kiume na Majandokasisi.  Na baadaye alikutana na Wawakilishi wa vyama vya kiraia kutoKa pande zote za dunia wakiwakilisha jumuiya za watu mbalimbali kijamii hasa maskini na wanaonyanyaswa na mifumo ya ubwanyenye na ukabila.

Katika mkutano Mapadre, Watawa na Majandokasisi, hotuba ya Papa ililenga zaidi katika somo la Injili ya Marko , juu ya  Bartolomayo, kipofu mwombaji.  Alisema , katika somo hilo mna mambo mawili makuu , kwanza kuna kilio cha mwombaji maskini Bartolomayo , na pili kuna jibu la watu  katika kilio hicho.  Baadhi ya watu walipita bila kujali na wengine walimtaka aache kulalamika na aondoke mahali hapo. Lakini Yesu alitoa jibu kwa subira, upole na fadhila.  Na Wanafunzi wa Yesu kama wakala wa Yesu, walimleta kipofu kwa Yesu kwa maneno ya kufariji na kumtia nguvu mpya.

Papa ametafakari hilo akisema ; hii ndiyo mantiki kuwa mwanafunzi wa Yesu,  ndicho ambacho Roho Mtakatifu anafanya juu ya maisha ya wanafunzi wa Yesu. Na wao kama viongozi wa kanisa  wanapaswa kuwa mashahidi wa uwezo, upole na saburi ya Yesu kwa watu wote. Papa alirejea katika wito wao akisema , siku moja Yesu aliwaona barabarani ,wakagaagaa katika maumivu  na taabu zao wenyewe. Yesu alitega sikio kwa kilio chao na kutoa jibu la la faraja lenye kuwatia nguvu katika kupambana na shida zao. 

 Papa aliendelea kutoa shukrani kwa ushuhuda mwingi uliokwisha tolewa na wengi, jinsi Yesu alivyo wainua na kutawala mioyo yao,  kuamka hatua kwa hatua, katika  uzoefu  wa upendo huu na huruma,  upendo wenye kubadilisha maisha , ambao huwezesha kuuona  mwanga wa maisha . Na pia wao , kama Mapadre, Watawa na majandokasisi , wanapaswa kushuhudia hilo si kama kichocheo cha itikadi ya teolojia pekee, lakini hasa  mashahidi wa uponyaji ,  upendo  na huruma ya Yesu, inayoonekana katika maisha yao na katika  maisha ya jumuiya zao.

Katika sehemu ya pili , Papa alilenga zaidi katika uwezo wa Injili  wa kubadili na kuponya mioyo, na kwa njia ya matendo ya watu nyoyo ya watu  zimeweza kugeuka na kuponywa ,  kubadilika na kuponya jamii na dunia waliyo pewa dhamana ya kuiongoza.

Papa aliendelea kusisitiza  kwamba, utume wao iwe  kwa ajili ya kufanikisha mgao mzuri wa matunda ya nchi na kazi ya binadamu,  siyo kama hisani tu, bali ni wajibu wa kimaadili.  Na kwamba  kwa Wakristo, wajibu  huu ni muhimu zaidi, maana ni  amri ya Yesu mwenyewe,  kuwapa maskini na watu kilicho chao kwa  haki.  Na kwamba uwepo wa mali za dunia isiwe tu katika wingi wamaandishi na takwimu, lakini kama ilivyolezwa katika mafundisho ya Kanisa ya jamii kwamba hasa ni hali halisi katika umiliki wa  mali binafsi.  Umiliki wa mali, hasa wenye kugusa  maliasili, iwe kwa ajili ya  kufanikisha  mahitaji ya watu. Na mahitaji hayo isiwe tu  matumizi lakini pia kudumisha yalipo.  Papa ameeleza na kuhimiza  wenye navyo kutoa kwa moyo wa ukarimu kwa maskini na si udondoshaji wa ziada katika kikombe cha maskini kinapotikisika ambacho kamwe kwa juhudi zake mwenyewe hawezi kukijaza.

Aidha Papa ameasa kwamba,  mipango ya kijamii peke yake haitoshi  na wala  uwezo wake wenyewe hauwezi  kuhakikisha utendaji wa kweli  na taratibu za adilifu katika  maisha katika jamii, isipokuwa kwa kuwa na sera na  mipango iliyosimikwa katika heshima, uhuru ,  ubunifu na  kazi shirikishi. Huo ndio ukweli wa dhati katika huduma kwa manufaa ya wote.








All the contents on this site are copyrighted ©.