Vatican Radio)Baba Mtaktaifu Francisco , Jumatano baada ya hafla ya mapokezi katika Uwanja wa Kimataifa la La Paz na kukutana na Rais katika Ikulu ya Bolivia ambako alipata muda wa kuwa na mazungumzo ya faragha na Rais Evo Morales Ayma, alielekea katika Kanisa Kuu la mjini La Paz, ambako alikuwa na ratiba ya kukutana na viongozi katika Mamlaka za kiraia na Wawakilishi wa tamaduni na vyama vya kiraia Bolivia.
Katika hotuba yake iliyokuwa imeandikwa tayari, Papa Francisko , kwa mara nyingine arudia kuzungumzia haja ya sera, mipango na kazi za serikali na taasisi mbalimbali kulenga kufanyika kwa manufaa ya wote na katika kukabiliana na changamoto zinazokabili jamii, hasa migogoro ndani ya familia, uhamiaji, na maendeleo endelevu kwa binadamu, na changamoto katika uwakilishi na viumbe.
Papa aliionyesha furaha yake ya kukutana na viongozi hao, kama nafasi makini ya
kushirikisha uzoefu wa utendaji kwa manufaa ya wote. Na pia kwa namna yakipekee alimshukuru
Askofu Mkuu Edmundo Abastoflor wa Jimbo Kuu la La Paz kwa makaribisho yake mazuri,
na wao kumpa ruhusa kutoa maoni yake kwa kifupi,kuwatia moyo na kuunga mkono kazi
zao.
Hotuba ya Papa ilianza na wito kwamba, kila mmoja wao mahali hapo ameitwa kufanya
kazi kwa ajili ya mazuri ya wote. Na alikumbusha kwamba Mtaguso Mkuu wa pili wa Vatican
uliochapishwa miaka hamsini iliyopita unatoa ufafanuzi bayana juu ya kufanya kazi
kwa manufaa ya wote, kama sharti msingi katika maisha ya kijamii ikiruhusu vikundi
vya kijamii na wanachama wake binafsi,katika uhakika na utayari wa kufanikisha malengo
yao wenyewe. Papa alieleza na kushukuru kazi na malengo yao, yanayowezesha watu
binafsi na jamii kwa ujumla , kuendeleza na kutimiza yanayotakiwa.
Na akaonyesha imani yake kwamba, wataendelea kwa uhakika, kupania ufanikishaji wa mazuri kwa manufaa ya wote, kupitia huduma ya kazi zao. Na aliombea juhudi hizo ziweze kutoa mchango mkubwa zaidi katika kuheshimu utu wa mtu , uliofumbatwa katika misingi inayohamasishwa na utendaji wa haki katika maendeleo endelevu, na umuhimu wake, katika ujenzi wa amani katika kijamii yenye utulivu na usalama kama inavyotakiwa na sheria za nchi , ambazo haziwezi kufanikishwa bila kujali kwa namna ya kipekee uwepo wa haki kwa watu wote.
Hotuba ya Papa iliendelea kutazama kwa makini umuhimu wa kujali utetezi na utunzaji wa mazingira kama hoja msingi pia katika maendeleo endelevu ya jamii hasa katika mtazamo wa mahusiano yake ya karibu katika miundo ya mazingira ya asilia na mazingira ya kijamii, kisiasa na kiuchumi. Papa amelitaja hilo kuwa jambo la dharura kwa kila mmoja wao, kutoa kipaumbele katika misingi ya kudumisha viumbe na mazingira katika asili zake, kama moja kipimo katika uwezo binadamu kuheshimu mazingira katika utatuzi wa masuala na changamoto za kijamii na mazingira katika nyakati zetu. Vinginevyo, Papa ameasa, matabaka ya barafu milimani yataendelea kupungua siku hadi siku. Papa ameeleza na kutoa shukurani kwa wale wote wanaofanya kazi ya kutetea wajibu kwa kuzingatia karama hizi, kama hatua ya kuhakikisha dunia inabaki katika mazingira yake asilia hata kwa vizazi vijavyo.
Papa ameeleza na kukumbusha kwamba kila jambo hutegemea jambo jingine na tunahitajiana mmoja kwa mwingine. Na akaonya dhidi ya sera za kisiasa kuongozwa na kigezo cha upatikanaji wa faida za kifedha , au uchumi kutawaliwa na mfumo wa ubingwa au kutafuta faida kwa kuongeza uzalishaji wa kiwango cha juu, bila kujali athari zingine kwa dunia na ubinadamu. Papa anasema , mazingira asilia yana uhusiano wa karibu na maisha ya jamii, kiutamaduni, kisiasa na kiuchumi pia.
Kwa maelezo hayo aliwageukia Wakristo akisema wao kama wafuasi wa Injili, waenezaji
wa Habari Njema na kama wajumbe wa wokovu wa binadamu , kwa namna ya kipekee wanatakiwa
kuvuvia na kuhamasisha uadilifu katika hayo. Na hivyo wanapaswa kushiriki katika
uongozi wenye njia za utendaji zenye kujali yote, maslahi ya mtu binafsi, na pia
kwa ajili ya manufaa ya wengine, kuwa na moyo wa kiasi, fadhila na wema kwa wengine,
katika mfumo wa kuishi kwa ushirikiano kama inavyosema Injili .
Hotuba ya Papa iliendelea kutazamisha katika hali za kileo ambamo watu wengi wamemezwa
na mazingira ya ukosefu wa usawa na moyo wa kutojali wengine. Uwepo wa mafanikio
yanayoelekezwa tu katika utajiri wa mtu mmoja kulimbikiza mali binafsi na tabia zauchoyo
na umimi, sera za kulinda maslahi binafsi kwa migongo ya wengine, badala ya kuwa na
njia za kueleweka katika mafanikio. Papa ametaja tabia ya ubinafsi, hufungua njia
ya mianya ya migogoro na migawanyiko ya kijamii;na hasa milango ubaya wote wa rushwa,
ambayo huvunjika moyo wanyonge na kuleta uharibifu kwa wengine . Utendaji unaomhamisha
mtu kujiweka mbali na utumishi kwa manufaa ya wote na kujikita katika ubinafsi na
umimi.
Pia Papa amezungumzia makundi mbalimbali ya kijamii yanavyokuwa na wajibu wa kufanya kazi kwa umoja na ushirikiano katika maendeleo ya jamii, akihimiza uzingatia wa uhuru wa maoni kwa wasomi, vyama vya kiraia na vyombo vya mawasiliano kwa ajili ya ufanikishaji wa sera na utendaji wa shughuli za wote kwa uwazi , upendo na ubunifu katika huduma kwa manufaa ya wote.
Katika hilo, Papa amewaasa Wakristo kwamba wameitwa kuwa chachu katika jamii,
kupeleka Injili ya upendo na mshikamano kwa manufaa ya wote.Amesema , Mwanga wa Injili
ya Kristo si mali ya kanisa; lakini ni Kanisa katika huduma ya Injili, inayoweza
kufikishwa katika miisho yote ya dunia. Imani ni mwanga wenye kuwamulikia wote hata
viongozi kuheshimu dhamiri na historia ya kila mtu na jamii. Ukristo una jukumu muhimu
katika kuchagiza utambulisho wa watu Bolivia. Ni changamoto inayolenga katika kusaidia
kukuza ukuaji wa kiroho na dhamira ya Kikristo katika miradi ya kijamii.
Papa alieleza na kutaja makundi mbalimbali ya kijamii, na hasa familia, ambayo ni
kila mahali hukutana na kitisho na unyanyasaji wa majumbani kutokana na , ulevi,
ngono, madawa ya kulevya, ukosefu wa ajira, kukosekana kwa utulivu wa mijini, kutelekezwa
ya wazee, na watoto mitaani. Matatizo haya mara nyingi, anasema Papa yameonekana
kuwa matokeo ya mifumo ya itikadi za ukoloni .. Hivyo matatizo mengi ya kijamii yanabaki
kutatuliwa kimya kimya ndani ya familia; na familia zikishindwa kuingilia kati familia
zingine, na hasa wale ambao wako hatarini zaidi na wasiokuwa na utetezi.
Papa ameitaja Bolivia kuwa iko katika njia panda ya kihistoria: kisiasa na kitamaduni
, na kidini, kama sehemu ya changamoto kwenye kukuza umoja na mshikamano , kwa taifa
hili ambalo historia yake ya nyuma iligubikwa na unyonyaji,choyo na aina zingine za
ubinafsi na utengano. Na kwa sasa unakuwa ni wakati kwa ajili ya kujenga upya umoja
na mshikamano. Papa ameonyesha imani yake kwamba, leo hii Bolivia inaweza "kujenga
aina mpya ya utamaduni wake wa awali. Kukishinda kigugumiza cha kutoaminiana, na
kuishi sera za ushirikiano na umoja hata na wale wanaoonekana kuwa tofauti, kwa
sababu mpya za maendeleo(Taz Evangelii Gaudium, 210).
Papa alihitimisha, kwa kumwomba Bwana ili taifa la Bolivia, liweze kupiga hatua kubwa za maendeleo endelevu yenye kuleta furaha kamili na baraka na amani kwa watu wake wote wa Bolivia . Na ameliweka taifa lote la Bolivia chini ya usimamizi na msaada wa Mama Bikira Maria. Na kuwasihi pia wamkumbuke katika sala zao.
All the contents on this site are copyrighted ©. |