2015-07-08 12:08:00

Hotuba ya Papa kwa viongozi wa Kisiasa , Wachumi na viongozi wa vyama wa kiraia


Jumanne , Baba Mtakatifu alikamilisha siku kwa kukutana na kundi la wanasiasa, wachumi na viongozi wa vyama vya kijamii, waliokuwa wamekusanyika katika kanisa la Mtakatifu Francis la mjini Quito .

Katika salaam zake Papa alitoa shukurani za dhati kwa kumfanya kuwa mmoja wa wakazi wa Quito, kwa Meya wa mji wa Quito , kumpatia fungua za  mji, kama ishara ya kuwa mmoja wao. Amesema hii ni heshima kubwa kwake iliyomfanya ajisikie nyumbani.  Na ni kielelezo cha upendo ukaribu, uliomfungulia milango yao kwake , na kumruhusu kusema machache juu ya funguo zingine za maisha , funguo katika maisha ya kijamii, kuanzia  maisha ya familia.

Hotuba ya Papa , ililenga katika jinsi kila mtu na kila kundi la kijamii linavyofurahia  kuwa  nyumbani. Amebainisha kwamba, katika familia, wazazi, mababu na watoto hujisikia nyumbani;  na ndani ya familia hakuna anayetengwa.  Hata kama kuna mtu mwenye  tatizo, hata matatizo makubwa, familia nzima hujali tatizo la mmoja wao na wote hushirikiana,  kujaribu kupata ufumbuzi wa tatizo linalokabili mwenzao. Papa anasema tatizo na mwanafamilia mmoja hivyo linakiwa ni tatizo la familia nzima na si hivyo tu, pia huwa ni tatizo la jamii inayomzunguka.

Kwa uzito huo, Papa Francisco alihoji juu ya maisha ya kifamilia katika mahusiano ya kijamii na maisha ya kisiasa, ambamo sasa kwa mara nyingi yamekuwa yakijengwa katika misingi ya mapambano na majaribio ya kuondoa  Wapinzani. Amekumbusha kuwa , katika familia, kila mmoja huwa na uchaguzi wake katika madhumuni ya kawaida, lakini utendaji huo hufanyika kwa manufaa ya wote. Hii haina maana ya kukataa utendaji binafsi wa kila mtu, lakini bali ni kuimarisha utendaji huo katika moyo kueleana na kuinuana na kusaidiana, katika yote  furaha na huzuni, kwa ajili ya wote.  Hiyo ndiyo  maana ya familia! Papa alieleza na kuonyesha hamu yake jinsi inavyowea kuwa na manufaa katika kuwaona wapinzani kama vile ni watoto ndani ya familia, au mke , mama au baba akisema kwa hakika pasingekuwa na matatizo katika jamii. Upinzani huo unakuwa hoja ya kujengana katika upendo zaid kati ya  jamii na kati ya nchi. Ni kupenda si kwa maneno tu lakini kwa  matendo pia.  Kwa  kila mtu, na katika kila hali, ni lazima kulenga katika maisha ya pamoja,  maisha ya upendo yenye kuongozwa  daima mawasiliano ya kujenga na si kutengana.

Papa alieleza hisia zake juu umuhimu wa familia kama kiini kikuu cha jamii katika ukweli kwamba , katika familia, tunapata maadili msingi ya upendo, udugu na kuheshimiana, ambayo hutoa tafsiri muhimu katika uadilifu wa jamii kwa ujumla:  moyo wa shukrani, mshikamano na kutegemeana.  Papa anawaona wazazi kama walimu wa kwanza msingi katika maisha ya mtu , akisema upendo wa wazazi kwa watoto wao  husaidia sana watoto  kuondokana na ubinafsi, husaidia watoto kujifunza kuishi na wengine, katika yote ,wakati wa neema, au wakati wa shida na taabu na pia katika kuwa na subira. Na kwamba katika maisha mapana ya kijamii , tunaweza kuona wema kama si jambo la ziada lakini kama jambo msingi katika utendaji wa haki, kwani mazuri yote ya dunia ni kwa manufaa ya wote.

Maoni ya Papa , yalielekea pia katika utajiri asilia wa Ecuador , akisema ,  utajiri asilia wa Ecuador ni kwa kila mtu na hivyo unakuwa ni wajibu  kuelekeza jamii kwa ujumla, kutunza maliasili hiyo pia kwa ajili ya vizazi vijavyo. Hatuwezi kurithisha urithi huu kwao bila huduma nzuri kwa mazingira, bila hisia ya ufadhili na uzalendo wa kuendeleza yaliyoumbwa katika  dunia hii.  Papa alieleza na kuelekeza mawazo katika misitu maarufu ya Equatorial Amazon, eneo  tajiri  kwa viumbe mbalimbali mimea na wanyama pia wanaopaswa kulindwa na kudumisha kwa ajili ya vizazi vyote vya leo na kesho.

Maelezo ya Papa , yametahadharisha  kwamba bila kuwa na mikakati thabiti , katika kipindi kifupi kijacho, maeneo asilia nyeti na viumbe wake yanaweza toweka  Ecuador  na katika  nchi nyingine zinazopakana Amazon. Papa ameasa , Tumepokea dunia hii kama urithi kutoka vizazi vilivyopita, lakini pia kama dhamana kwa ajili ya vizazi vijavyo, Na hivyo tunapaswa kukabidhi kama tulivyopokea.  

Papa ameeleza Ecuador, kama mataifa mengi ya Amerika ya Kusini, sasa yanakabiliwa na mabadiliko makubwa ya kijamii na kiutamaduni,  changamoto mpya inayokabili kila sekta ya jamii, ikiwa ni pamoja na  Uhamiaji,  msongamano katika miji mikubwa, ulaji, migogoro katika familia, ukosefu wa ajira na mfumko wa umaskini: Sababu hizi zote hujenga uhakika wa mivutano yenye kutishia amani ya kijamii. Sheria na kanuni, pamoja na mipango ya kijamii, kwa sasa inajenga  haja  kujenga fursa sawa katika  mazungumzo na mikutano, wakati kuacha nyuma ya aina zote za ukandamizaji, na udhibiti mkali au kupoteza uhuru wa kuwa na kumbukumbu katika  maumivu nyuma. Ni muhimu na lazima kuwa na mipango ya kujenga matumaini mapya bora, kama fursa halisi kwa watu, hasa watu vijana,  pia  kujenga ajira, na ukuaji wa uchumi wenye kuhakikisha ushiriki wa wote kimatendo na si katika maandishi yaliyopo kwenye  karatasi, au katika takwimu za uchumi). Mtazamo ni lazima iwe  katika kukuza maendeleo endelevu na uwezo wa uzalishaji  imara na mshikamano thabiti kijamii.

Ili hatimaye, heshima kwa watu wengine, heshima tunayojifunza katika familia, ipate kuonekana katika maisha ya kusaidiana kijamii. Ni kuwa na utambuzi kwamba, uchaguzi wetu si lazima tu uwe ndiyo tu  halali lakini liwe ni pendekezo linalotolewa kwa  unyenyekevu, katika  kutambua wema asili kwa  watu wengine, hata kwa mapungufu yao na tofauti  za uwezo wa kihali.  Watu binafsi na vikundi wana haki ya kwenda njia zao wenyewe, hata kama wanaweza wakati mwingine kufanya makosa. Kwa ajili hiyo, vyama vya kiraia vinaitwa kusaidia kila mtu na mashirika ya kijamii kuchukua nafasi yake na maalum, katika kutoa mchango wake kwa manufaa ya wote. Kwa ajili ya kufanikisha hili mazungumzo yanahitajika kama  jambo la msingi katika kuwasilisha ukweli, katika msingi wa demokrasia  shirikishi, kwa  kila kundi kijamii, wenyeji, wazawa wenye asili ya Afrika,  Afro-Ecuadorians, vyama vya kiraia na wale wanaohusika katika utumishi wa umma,  wote  na wawe washiriki muhimu katika mjadala huu.

Baba Mtakatifu Francisco ameeleza na kutaja matakwa ya kanisa kwa upande wake, kuwa ni  kushirikiana katika harakati zote kwa manufaa ya wote,  kupitia shughuli za kijamii na kielimu katika  kukuza maadili kwa yote  kiroho na kijamii pia, na utume wake wa kuwahudumia kama ishara ya kinabii katika kutoa miali ya  mwanga wa  matumaini  yote, hasa kwa wengi wahitaji .

Papa alieleza na kuwashukuru wote kwa kumsikiliza. Na aliwaomba maneno yake yabaki ndani ya mioyo yao kama  faraja kwa jamii mbalimbali na makundi  yaliyowakilishwa katika mkutano huo. Na alimwomba Bwana awajalie neema zake ili kwamba jamii wanayo wakilisha   daima iweze kuwa na mipango yenye  utendaji  wa kufaa kimaadili kwa hayo aliyoyazungumza. 








All the contents on this site are copyrighted ©.