(Vatican Radio) Jumatatu, Papa Francisko akiwa katika siku ya Pili ya ziara yake ya Kitume Amerika ya Kusini, majira ya asubuhi aliongoza ibada yake ya kwanza hadharani, katika mji wa Guayaquil Equador, ibada iliyohudhuriwa na umati wa watu zaidi ya milioni moja. Homilia yake ililenga kuwatia nguvu waamini kwamba kila tunaposali na kunyanyua sauti zetu kwa Mungu hofu na mashaka yetu huondolewa . Sala huyahuisha juu ya yote yanayotuumiza au kuudhi au kutufadhaisha. Maombina sala hutuweka katika nafasi yakujali pia mahitaji ya wengine.
Baba Mtakatifu alieleza hilo wakati akitoa tafakari juu ya muujiza wa Kana , muujiza wa kwanza wa Yesu, alipogeuza maji kuwa mvinyo, kama ilivyoelezwa katika somo la Injili ya Yohana , ambamo Mama Maria anaonyesha kujali mahitaji ya watu na kuomba kwa Yesu akisema ; watu hawana mvinyo, na Yesu anatoa jibu akirejea saa ya mateso yake.
Ishara ya muujiza wa Kristo huko Kana - kugeuza maji kuwa mvinyo , Papa anasema,
inaonyesha jinsi Mama Maria, anavyojali mahitaji yetu. “Mama Maria alikuwa makini,
na aliweka hofu na mashaka yake kwa Mungu na kutenda kwa uangalifu na ujasiri."
Sura hii ya Maria katika kujali mahitaji ya Maarusi huko Kana , Papa Francisko alisema,
inaonyesha jinsi Maria alivyojali mahitaji ya wengine, Maria hakujifungia binafsi
katika shida zake, lakini alijali pia mahitaji ya wengine. Papa aliianisha hali ya
wakati huo wa Arusi ya Kana na hali nyingi zinazoonekana leo hii, kwamba "mvinyo"
inakuwa ni ishara ya furaha, upendo, na mengine mengi kutokuwepo. Alihoji , ni
vijana wetu wangapi wanaojisikia hawana makazi? Na ni wanawake wangapi wanaobaki
wamemezwa na hali ya huzuni na upweke baada ya kupoteza wapendwa wao au wakati hali
za kijikimu kimaisha zinapokuwa mbali nao? Na ni wazee wangapi, wanaotelekezwa nje
maadhimisho ya kifamilia, kutupwa kando na kila siku wakitamani walau kupata upendo
kidogo? "
Papa alijibu hoja hizo kwa kurejea utendaji wa Mama Maria katika Injili, jinsi
alivyojali mahitaji ya wengine , alivyotafuta jibu katika kukosekana kwa mvinyo.
Alimwendea Yesu kwa ujasiri, na kuomba. Papa Francisko anasema, Maria anatufundisha
kuweka familia zetu mikononi mwa Mungu, kuomba, kuwasha matumaini mapya wakati tunapoona
kuna matatizo, kuna upungufu. Ni kuweka wasiwasi wetu kwa Mungu. Na sala na maombi
, aliendelea, daima hutuhuisha nje ya wasiwasi na mashaka yetu.
Homilia ya Papa iliendelea kuitaja familia kama shule ya sala , kama yalivyokuwa maneno
ya Maria kwa wahudumu wa arusi , lolote atakalowaambia fanyeni. Baba Mtakatifu anasema
, huu pia ni mwaliko kwetu kufungua mioyo yetu kwa Yesu, aliyekuja kutumikia na siyo
kutumikiwa. Na kwamba katika mfano huu sisi tunajifunza kuwa ndani ya familia ni kuwa
watumishi wa mtu mwingine, na ni mahali ambamo hakuna anayekataliwa. Familia ni
mtaji bora wa kijamii". Familia haina mbadala, na haiwezi kulinganishwa na taasisi
nyingine. Papa Francisko alisisitiza na kutoa mwaliko wa nguvu kwa jamii kutetea
familia, akisema ni lazima familia isaidiwe na kuimarishwa."
Familia, aliendelea kusema, pia ni "Kanisa dogo, 'Kanisa la ndani' ambamo, pamoja
na maisha, pia ni mjumbe wa huruma na huruma ya Mungu. Pamoja na familia zetu wakati
mwingine kuwa nje ya mategemeo yetu , au kuwa na picha mbaya tusiyotegemea hata hivyo,
kila siku ndani ya familia hapakosekani miujiza kwa madogo yanayofanyika. Katika
familia zetu wenyewe na katika familia mkubwa ambamo sisi sote tunahusika, hakuna
anayepaswa kutekelezwa kando, au wa kuonekana kama hana thamani. Papa Francisko
alieleza na kuomba sala kwa ajili ya Sinodi juu ya familia, ili Kristo anaweza kuyabeba
yote , hata yale yanayoonekana kwetu kutofaa, kashfa, au vitisho, na kuyageuza kuwa
miujiza.
Papa amesema , ni jambo jema kujua jinsi Yesu anavyoguswa na mahitaji yetu . Na hivyo
tunapata kujua kwamba Yeye daima yu pamoja nasi wakati tunapopungukiwa, wakati wa
dhiki na katika furaha pia . Papa alielezana kurejea ombi la Maria kwa Yesu , hawana
Mvinyo. Pamoja na mfano wa Maria katika kujali mahitaji ya wengine pia Papa alirejea
mifano wa maisha watakatifu Narcisa na Mercedes , akisema si kazi ngumu kuyaiga maisha
yao iwapo tutakuwa na Mungu ndani mwetu. Wao walitimiza kazo yao na wanatuonyesha
hakuna kinacho shindikana iwapo tu pamoja na Mungu. Wanatuonyesha upendo wao mkuu
kwa maisha ya wengine , maisha ya kila siku wakiguswa na mateso ya mwili wa Kristo
kwa wengine., kama ilivyoelezwa pia katika Waraka wa Kichungaji wa Injili ya Furaha.
Papa anasema, watakatifu hawa hawakufanya kazi zao kwa kujifungia wenyewe binafsi , lakini walitenda kwa kushirikiana na wengine , ili kwa njia hiyo , inakuwa ni njia yetu sote , njia asilia , kutenda katika hali ya ukimyakimya sambamba na jamii , kwa manufaa ya jamii nzima bila kutafuta faida binafsi au sifa binafsi .
Ukosefu wa Mvinyo amefafanua Papa Francisko unaweza kuwa ukosefu wa ajira, ukosefu wa afya za kimwili, au uwepo wa mapungufu katika hali zingine za maisha. Mama wa Yesu hakudai kwa nguvu lakini alionyesha kwa upendo upungufu uliokuwepo .
Baba Mtakatifu alihitimisha hotuba yake kwa kuonyesha ukweli kwamba, wakati wa harusi ya Kana, yaliyo mazuri zaidi yalikuwa bado kutolewa kwa ajili ya familia. Kama Mungu alivyokwisha sema , tafuteni nanyi mtapata , daima ni kutafuta hadi pembezoni, wale walioishiwa na mvinyo , wale wanao wanaotafuta kinywaji , baada ya kuishiwa , wale waliokata tamaa . Yesu anausikia udhaifu wao , na kutoa mvinyo ulio bora zaidi hata kwa wale wanaosikia kuvunjika moyo.
All the contents on this site are copyrighted ©. |