2015-07-07 15:16:00

Neno la Mungu linatutaka kuishi katika umoja


Jumanne 7 Julai, ikiwa siku ya tatu ya ziara yakeya kitume  Amerika ya Kusini akiwa bado Equador, Baba Mtakatifu Francisco majira ya asubuhi  kwa saa za huko, aliongoza Ibada ya Misa katika uwanja wa Bicentenary wa mjini Quinto, uwanja  uliozinduliwa rasmi tarehe 27 Aprili 2013. Uwanja uliopewa jina la Bicentenary kwa heshima ya kumbukumbu juhudi za kihistoria, za watu mahalia wa Equador , kudai uhuru wao. Kilio kilichotokana na ukosefu wa uhuru, unyonywaji na ubwanyenye .

Katika Ibada hiyo, Papa Francisko, amewasisitizia waamini kwamba, Neno la Mungu linawahitaji waishi katika umoja, ili ulimwengu upate kusadiki.

Papa ameonyesha hamu yake, kuona vilio hivi, vinaunganishwa chini ya uzuri wa uinjilishaji kama changamoto. Papa ameasa kwamba, kuinjilisha hakuhitaji kutumia maneno mazito mazito au dhana ngumu, lakini maneno mepesi yenye kuonyesha furaha ya Injili", furaha yenye kuijaza mioyo na maisha ya wote wanaokutana na Yesu katika Injili yake ya upendo. Kwa wale ambao hukubali mwaliko huu wa kukombolewa, Papa anawathibitishia kuwekwa huru dhidi ya dhambi , huzuni, utupu wa ndani na upweke. Aidha wote wanaokusanyika  mbele ya meza ya Yesu ni watu wa kawaida, ambao ni sisi wenyewe,  tunaotoa kilio cha ukelele wa imani katika uwepo wa Yesu mwenye kuongoza katika umoja, akionyesha upeo mzuri  na mwaliko kwa wengine, ili pia washiriki katika karamu yake nzuri. .

Baba Mtakatifu ameeleza na kurejea  ombi la Yesu Mwenyewe kwa Baba yake , “Baba  naomba wawe  kitu kimoja ... ili  ulimwengu upate kuamini".  Na kwamba sala hii ya Yesu, ni sala ya kitume: "Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami pia nimewatuma wao ulimwenguni". Yesu kwa wakati huo alikuwa akiishi uzoefu wake mwenyewe katika uchungu wa maisha ya dunia hii , dunia aliyoipenda kwa upendo mkuu, hata kukubali kuyatoa maisha yake mwenyewe ili ulimwengu upate kukombolewa dhidi ya dhambi. Licha ya kujua kikamilifu maovu, uongo na usaliti wa dunia, kujua yatakayomkabili mbele, hakusita  wala kulalamika juu ya  utume wake, bali aliendelea kutimiza mapenzi ya Baba yake.Na ndivyo sisi pia tunavyokutana na matatizo katika maisha yetu ya kila siku, tunakutana na dunia iliyosambaratishwa na vita na  vurugu.  Inakuwa ni kujidaganya kufikiri  kwamba,  mgawanyiko na chuki ni matokeo ya mapambano kati ya mataifa au kati ya vikundi vya  jamii. Lakini hayo ni matokeo ya kuenea kwa ubinafsi , wenye kututenganisha sisi na kutuweka mbali na wengine,  mmoja kwa mwingine. Ni urithi wa dhambi  uliomo katika moyo wa binadamu, wenye kuleta mateso makubwa katika jamii na viumbe wote. 

Baba Mtakatifu ameendelea kuieleza hali ya kidunia leo hii  akisema hakuna kinacho punguza  imani au nguvu katika kilio cha uhuru kilichotolewa zaidi ya miaka mia mbili iliyopita . Hali bado ni ileile na njia pekee inayoweza kuwaunganisha watu na kuwapa matumaini ni Uinjilishaji . Hili tuna  imani nalo na tunaweza kupaza kilio chetu juu yake., kama ilivyokuwa kwa baadhi ya mataifa yanayoziishi hali za mizozo na vita,  ambako Wakaristo wamebaki kuwa nguzo imara katika kutoa angalisho la kujali wengine , kuponya makovu yao na kujenga madaraja na kuimaeisha uhusiano na kubebeana mizigo ya matatizo .Hamu ya kuwa na umoja imefumbatwa katika furaha ya kuinjilisha na katika kishawishi cha imani kwamba ni hazina tunayopaswa kushirikishana  na kugawana na kukua ndani mwake kwa ajili ya manufaa ya wote. Ni katika dunia hii  yenye matatizo ambako Yesu anatutuma sisi kwenda. Na ni lazima tutoe jibu katika wito wake bila malalamiko wala kudai kwamba hatuna vitendea kazi , au kwamba matatizo hayo ni magumu mno kwetu. Badala yake , ni lazima tutoe jibu kwa kukichukua kilio cha Kristo kwa kuikubali neema yake na changamoto ya kuwa wajenzi wa umoja. 

Hotuba ya Papa iliendelea kukilinganisha kipindi hicho cha karne 2 zilizopita akisema, hapakuwa na upungufu katika ushawishi au nguvu ya kilio cha kudai uhuru.  Na historia inatuonyesha sisi kwamba, iliwezesha kusonga mbele na watu waliweka kando tofauti zao na kwa pamoja kwa hamu ya madaraka na uwezo wa kutenda,  walifurahia uwepo wa vyama vya kutafuta uhuru ambavyo vilikuwa tofauti lakini vikiwa na lengo moja bila kupingana. 

Kwa mtazamo huo Papa aliendelea kueleza kuwa, Uinjilishaji unaweza kuwa njia ya kuwaunganisha watu katika matumaini , katika kujali na katika kuwa dhana hata katika hali za kufikirika. Papa alionyesha imani yake katika hilo kwamba hicho ndicho kilio chetu leo hii. Papa alieleza kwa kurejea katika dunia yetu leo hii na hasa katika baadhi ya mataifa, yanayokabiliwa na aina mbalimbali za mifumo ya kivita na mizozo inayoibuka upya , ambako Wakristo wanabaki kuwa kielelezo imara katika kujali mahitaji ya wengine, na  katika kuheshimu wengine, kuponya makovu yao ya kiroho na kihali , na katika kuwa wajenzi wa madaraja kati ya watu na katika kuimarisha mahusiano na katika kubebeana mizigo ya matatizo mmoja kwa mwingine.

Hamu ya kuwa na umoja wenye kuhusiana na furaha na faraja ya kuinjilisha. Ushawishi wenye kuchipuka katika hazina ya umoja na hamu ya kuwagawana vilivyoko, utahabiti wa moyo unaotokana na hoja makini ya kujali mahjitaji ya wengine, ikijenga hamu ya kufanyakazi kwa ushirikiano katika kila ngazi na kufuta kila aina ya ubinafsi na choyo badala yake kujenga daraja la majadiliano na ushirikiano. Papa ameasa kwamba, tunahitaji kutoa mioyo yetu kwa ajili ya wenzu  wetu tunaotembea pamoja nao katika njia hii bila ya kuwatilia mashaka au kutowaamini.  Ni kuwa na imani na  wengine kuwa ni imani ni  sanaa na amani ni sanaa. Na kwamba umoja wetu hauwezi kung'ara iwapo roho ya kidunia itatufanya sisi kuonea wengine wivu katika kiu hii ya  mamlaka na  usalama wa kiuchumi. 

Papa ameuita umoja na ushirikiano huo, kuwa  tayari ni kitendo cha kitume , ili dunia ipate kusadiki. Na kwamba,kuinjilisha haina maana ya kurubuni au kulazimisha wengine, lakini ni mvuto unaotokana na  ushuhuda wa waamini wa kuvutia waliombali, na kwa unyenyekevu kuwaleta karibu, wale wote  wanaojisikia kuwa mbali na Mungu na kanisa au wale wenye kuwa na hofu au kuwa tofauti na kusema kwao,  Bwana pia anakuita kuwa sehemu ya watu wake na anafanya hivyo kwa heshima kubwa na upendo "(ibid, 113.). Huo ndiyo ujumbe wa Kanisa kama sakramenti ya wokovu, ni thabiti na ni utambulisho wa hoja  na wito, unaotakiwa kuingizwa katika maendeleo ya  mataifa yote ya dunia.








All the contents on this site are copyrighted ©.