2015-07-06 11:36:00

Kongamano juu ya Miito barani Ulaya leo hii


Katika Mji Mkuu wa Prague Czech,  Tume ya  Baraza la Mabaraza ya Maaskofu barani Ulaya CCEE, kwa muda wa siku tatu 6-9 Julai 2015, kunafanyika kongamano chini ya kauli mbiu : “ Jinsi ya Kuongozana na Vijana kuelekea Upadre na Maisha wakfu,katika mtazamo wa familia leo hii”.

Kongamano , ni katika mtazamo wa Mwaka wa Watawa na kilele cha Sinodi ya Maaskofu ijayo  juu ya  familia, kama ilivyoandaliwa na Tume CCEE kwa ajili ya huduma katika  miito barani Ulaya (EVS) pia kama tukio la mkutano wa  mwaka juu ya mandhari ya kuwasindikiza  vijana  wanaowania kuhani na maisha wakfu katika mazingira ya utamaduni wa familia  leo hii. Kongamano linafanyika Prague kwa mwaliko wa Mgr Josef Kajnek,  Askofu Msaidizi wa Hradec Kralove, nalinahudhuriwa na wajumbe  72, ikiwa ni pamoja na maaskofu tisa, pamoja na Wale wanaosimamia huduma za Kichungaji katika miito na wajumbe kutoka Mabaraza ya Maaskofu ya  Ulaya na Mabaraza ya kidini, kutoka mataifa 20 ya Ulaya na kutoka Tume ya Watawa kutoka Marekani.

Nia kuu la Kongamano  hili kufanyika tena Ulaya ni kutoa angalisho  katika  utendaji makini katika huduma za kichungaji kama kipaumbele muhimu kwa kanisa zima na kwa ajili ya huduma za kichungaji katika famillia na miito . Yaani, kujenga mazingira ya  miito katika  utamaduni wa familia, ili familia iwe kweli "kitalu” cha miito. Hii ina maana kwamba, familia si tu  mahali ambapo kipeo cha  elimu kwa nyakati zetu kimeibuka kwa kasi sana , lakini familia inaweza kuwa ni mahali pa upatanisho na miito mingine , na  hatua kwa hatua, kuwezesha  kuzaliwa moyo mpya wa kuanza  safari katika miito mbalimbali. 

Hayo yameeelezwa na  Mgr Domenico dal Molin, Mkurugenzi wa Ofisi ya Miito ya Baraza la Maaskofu  Italia , ambaye pia ni  mratibu wa Tume ya Miito ya CCEE-EVS.  Amesema  ,wanalenga hasa kuonyesha kwa namna ya kipekee,  umuhimu wa wazazi  kama chemichemi ya miito, iwapo wazazi watatimiza wajibu wao katika  malezi kwa watoto wanaojaliwa,  au kudhaminishwa pia  kwa niaba ya mashirika mengine ya  elimu, na hasa zaidi ya yote, katika kupambana na  ongezeko la uvamizi wa wingi vyombo vya habari. Na kwamba , wanataka kudumisha hazina na pembejeo zilizotolewa  na  Papa Francisco katika waraka wake wa Injili ya Furaha  '' “Evangelii Gaudium ', juu ya kuyatoa  maisha kama matunda ya  muungano na wazazi, ili kusaidia kugundua upya uzoefu wa wanandoa, kama kitalu cha elimu katika chaguzi za  maisha, hata kwa wale wenye kuwa na msimamo mkali kwa watoto wao.

Kongamano hili la  Prague, linafanyika chini ya uenyekiti wa  Mgr Oscar Cantoni, Askofu wa Crema (Italia) na Rais wa Tume ya Miito ya  CCEE-EVS. Kongamano linaendesha kwa vipindi vya hoja, vikundi kazi, na michango kutoka wanasosholojia,  Attilio DANESE na Giulia Paola Di Nicola pamoja majadiliano yenye kichwa "kusoma hali ya kijamii na kiutamaduni  kwa familia za Ulaya: vigezo na miongozo kwa ajili ya elimu katika imani na hali nzuri kwa ajili ya MIITO.  Hili litafuatiwa na tafakari itakayotolewa na  Mgr Wong, Katibu wa Usharika kwa ajili ya viongozi wa dini, chini ya jina "Jinsi ya kuongozana vijana katika  ukuhani na maisha wakfu katika mazingira ya familia ya leo."

Pia  Kardinali Dominik Duka OP, Askofu Mkuu wa Prague na Rais wa Baraza la Maaskofu Czech ' anatazamia kuhudhuria baadhi ya vipindi vya kongamano hili , ambalo majadiliano yake si wazi kwa umma,  hadi siku yake ya mwisho Alhamisi Julai 9 , ambako ujumbe wake wa mwisho utachapishwa katika lugha za Kiingereza, kifaransa , kijerumani na Kiitalino mapema siku ya  Ijumaa Julai 10. 

Kwa habari zaidi juu ya Kongamano hili zinapatikana katika CCEE tovuti (www.ccee.eu) na Huduma ya Miito Ulaya  - EVS (http://www.vocations.eu)

Na TJMHELLA, 

Idhaa ya Kiswahili , Redio Vatican 








All the contents on this site are copyrighted ©.