Umoja wa Mataifa umehimiza Serikali zote, kuharakisha juhudi za kufikia makubaliano juu ya utendaji kwa ajili ya kuokoa hali ya hewa , kabla ya Mkutano Mkuu juu ya mabadiliko ya Tabia nchi utakao fanyika Ufaransa Desemba ijayo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa , Ban Ki-moon , alitoa rai hiyo siku ya Jumatatu,
katika mkutano uliofanyika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa , uliolenga katika mabadiliko
ya tabia nchi. Katibu Mkuu alionyesha kujali kwamba ni muda mfupi umebaki kabla ya
mazungumzo ya viongozi kukutana katika mji mkuu wa Ufaransa, Paris.
Kwa mujibu wa Taarifa ya Stephanie Courtrix , Mkuu wa Umoja wa Mataifa alionyesha
kujali kwamba, masuala muhimu ya kisiasa, bado yako kwenye meza ya majadiliano ingawa
sasa , ni wakati kwa uongozi wa ngazi za juu kutoa jibu lake . Ban Ki-moon alisisitiza
kuwa ,safari ya jamii ya kimataifa inapaswa kwa ujasiri, kuchukua hatua madhubuti
za kuokoa hali ya hewa na wakati ni huu, ni muhimu kufanya hivyo, kwa ajili ya kuhakikisha
joto la dunia halipandi zaidi ya digrii 2 Celsius.
Kwa uchungu, Katibu Mkuu alionya “iwapo watashindwa kutekeleza yanayopaswa kuzuia
joto kupanda, basi wanajipalia mkaa wa laana kwa watoto wa leo na wajukuu wao,
kwa kuendelea mustakabali wa machafuko ya hali ya hewa. Lakini iwapo watafanikiwa
kudhiti joto, wataiweka dunia katika njia ya utulivu mkubwa, afya bora na nguvu ya
uchumi, kwa faida wote. Nchi zote zinaweza na lazima ziwe sehemu ya ufumbuzi.
Bwana Ban alionyesha imani yake kwamba, viongozi wa dunia katika mkutano wao wa Paris,
watapitisha makubaliano thabiti juu ya hali ya hewa, makubalinao ya maana yenye
kuwa na manufaa kwa watu wote. Na kwamba ni lazima kuazimia kushusha kiwango cha
uzalishaji wa hewa ya ukaa kwa siku za baadaye, kwa kuunga mkono uwekezaji katika
nishati safi na rahisi katika mabadiliko ya kukabiliana mabadiliko ya hali ya hewa
na malengo mpya kamambe kwa siku za usoni. Stephanie Coutrix, Umoja wa Mataifa, ametaarifu.
.
Aidha
Ijumaa iliyopita wa Mataifa, uliazimisha miaka70 tangu kuanzishwa kwake. Sherehe za kumbukumbu hii zilifanyika huko San Francisco Marekani, mji ambako mkataba wa Umoja wa Mataifa ulitiwa saini katika mji huo, na kuwa chombo hicho cha dunia, tarehe 24 Oktoba 1945, baada ya serikali katika nchi nyingi kuupitishwa mkataba.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon , alizungumzia jitihada jasiri za wakati
ule ambapo hamu ya kuwa na ulimwengu mtulivu na bora ulishinda Hofu ya vita vya Pili
vya Dunia. Kupitia mazungumzo makali, wajumbe waliweza fanikisha ndoto zao. "Kwa
kupitishwa kwa Mkataba huo , dunia iliweza kujifunua upya katika njia ya kutembea
pamoja. Katibu Mkuu alielezana kukumbuka kwamba wakati hayo yanafanyika yeye alikuwa
amezaliwa akiwa na miezi tu, na Umoja wa Mataifa, haukuchukua muda mrefu, kufanikisha
mabadiliko mema duniani kwa ajili ya wote.
Miongoni mwa maofisa wa Umoja wa Mataifa na na watu mashuhuri waliofika katika sherehe
hii ni pamoja na Malala Yousafzai wa Pakistan, Mshindi wa Tuzo ya Amani ya 2014,
ambaye Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, amemwita kuwa mwenge wa kizazi chake.
chanzo :Radio Umoja wa Mataifa .
Imetolewa na Tabitha Janeth Mhella
All the contents on this site are copyrighted ©. |