2015-05-17 14:14:00

Msingi wa imani ya Mkristo ni kumshuhudia Kristo Mfufuka


Papa Francisko akihubiri wakati wa Ibada ya Kuwataja Watumishi wa Mungu wanne kuwa Watakatifu, mifano ya maisha ya kuigwa na waamini wa Kristo, homilia yake alitafakari matendo ya mitume wakati Kanisa la mwanzo lilipochagua  mtu aliyeitwa na Mungu, kuchukua nafasi ya Yuda katika kundi la  Mitume. Alisema hili linaonyesha  utume wa kanisa si kama ni  kazi, lakini  hasa ni  huduma. Kwa hakika kama uchaguzi huo ulivyomwangukia , Matias, ilikuwa ni ushuhuda kama Mtume  Petro alivyofafanua kwa maneno haya: "Mmoja wa watu hawa ... lazima awe  mmoja wetu katika kushuhudia na sisi ufufuo wa Kristo (Matendo 1: 21-23 ). Kwa njia hii,  Papa alisema , Petro anavyohitimisha nini maana ya kuwa sehemu  Mitume kumi na wawilii: ina maana ya kuwa shahidi wa ufufuo wa Yesu. Katika  ukweli wake , pia hutuwezesha sisi kutambua kwamba, utume wa  kumtangaza Kristo Mfufuka  si utendaji wa  mtu  binafsi; lakini inapaswa kutekelezwa kwa pamoja, dekania ya Maaskofu na jumuiya  ya waamini.  

Papa alieleza na kutoa shukurani kwa nguvu ya ushuhuda uliotolewa na Mitume ambao walilishuhudia tukio la ufufuko wa Bwana kwa macho yao, walishuhudia hata wengi wakaamini na kuwa na imani kwa Bwana aliyefufuka, na hivyo kuzaliwa kwa  jamii ya Kikristo tangu wakati huo na siku zote wanaendelea kuzaliwa .

Papa aliweka bayana kwamba,hata kwetu sisi  leo, msingi wa imani yetu katika Bwana aliyefufuka, inahusiana na ushahidi wa Mitume, unao tufikia kupitia mafundisho ya Kanisa. Imani yetu inafanywa kuwa imara kutangaza ujumbe huo, kama mnyororo usioweza vunjika  katika mapito yote ya karne na karne, kukiundwa si tu warithi wa Mitume, lakini pia imani kwa vizazi kwa vizazi vijavyo vya Wakristo. Na hivyo kama ilivyokuwa kwa Mitume, hata leo hii,  kila mmoja kama  mfuasi wa Kristo,  anaitwa kuwa shahidi wa kufufuka kwake Kristo, na hasa kaika mazingira ambako binadamu anakuwa na mwelekeo kutaka kusahau  ukuu wa Mungu,  kuchanganyikiwa kwa  binadamu kunakoonekana dhahiri zaidi kwa nyakati hizi.

Papa Francisco ameeleza na kuwatahadharisha, Wakristo, kupambana  na hali hiyo kwa kushika imani yao  kwa Bwana Mfufuka kwa upendo thabiti zaidi, kama Mtume Yohana alivyowakumbusha waamini , Yeye aishiye katika upendo, anaishi katika muungano na Mungu, na Mungu hukaa ndani yake" (1 Yohana 4 : 16). Na Yesu  mara kwa mara  aliwasisitiza wanafunzi wake, "Kaeni ndani yangu ... Kaeni ndani yangu upendo" (Yn 15: 4, 9).  Papa ameitaja kuwa hii ndiyo  siri ya watu wa Mungu: kudumu ndani ya Kristo, kuungana nae kama matawi katika mzabibu, ili kuzaa matunda mengi (taz Yohana 15: 1-8). Na matunda haya si kitu kingine  ila ni  upendo. Upendo wenye kuangaza hadi nje, kama alivyoshuhudia  Mtawa  Jeanne Emilie de Villeneuve, aliyeyaweka masiha yake wakfu kwa Mungu na kwa maskini, wagonjwa, wafungwa  na  wanaodhulumika vibaya, akiwaendea wote na  ishara halisi za Bwana mwenye huruma na upendo.

Papa aliendelea kuainisha ushuhuda wa maisha ya Watakatifu wapya  kwa Bwana aliyefufuka, akitaja ushuhuda wa kila mmoja wao, kwamba ulichota nguvu kutoka kwa Bwana Mfufufo , katika kujenga umoja na upendo thabiti ,  kama  ilivyoeleza  Injili,  Ombi la Yesu katika usiku wa mateso yake: "ili wawe kitu kimoja kama sisi ni tulivyo wamoja" (Yn 17:11). Na upendo huu wa milele kati ya Baba na Mwana, hutiwa katika mioyo wa Mkristo na  Roho Mtakatifu (Rum 5: 5).

Hivyo Papa akatoa mwaliko kwa Wakristo wote akisema,  dhamira yetu na ushirika wetu wa kidugu ni kuteka nguvu katika upendo huu, wa Injili , hata katikati ya vikwazo na matatizo na hata kutoelewana .Upendo wenye kuutunganisha kama  yalivyokuwa maisha ya  Sista  Maria Chiristina Brado, alizama katika upendo wa kweli kwa ajili ya kumtumikia bwana wake.Na kupitia sala na kukutana na Kristo Mfufuka katika Ekaristi, aliweza kupata nguvu za kudumu katika mateso na kujikabidhi bila ya kujibakiza katika Mkate uliovunjwa kwa ajili ya kuokoa wengi  waliokuwa mbali na Mungu lakini wakati huohuo wakiwa na kiu kubwa ya kupata upendo wa kweli .  Yeye anakuwa mfano wa furaha yetu katika kumfuata Bwana katika njia ya umaskini, usafi wa moyo na  utii, upendo  anaotuita katika sala na tafakari. Usikivu wa Maria Brado licha ya kuwa maskini na asiye na kisomo, aliweza kuwa mshauri mzuri kwa wengine , na hata katika kukutana na  usharika na ulimwengu wa Kiislamu.

Na ndivyo ilivyokuwa kwa Sista  Marie Alphonsine Danil Ghattas,  alielewa wazi nini maana ya kutoa miali ya  upendo wa Mungu katika utume na huduma kwamba ni  kuwa shahidi wa upole na umoja. Yeye anatuonyesha umuhimu wa kuwa na kuwajibika kwa ajili ya mtu mwingine,  kuishi maisha ya kuhudumiana mmoja kwa mwingine.

Papa aliendelea kusema, kukaa ndani ya Mungu na katika upendo wake, na hivyo kutangaza kwa maneno yetu wenyewe na maisha yetu kufufuka kwa Yesu, inakuwa ni kuishi katika umoja na kuhudumiana kwa upendo unaowaelekea  wote. Hivyo ndivyo walivyofanya wanawake hawa wanne , waliotajwa kuwa Watakatifu leo hii. Kung’ara kwao katika maisha ya kuhudumiana inakuwa ni changamoto kwetu katika maisha yetu kama Wakristo.

Papa alihoji kwa vipi inawezekana  kumshuhudia Kristo aliyefufuka? Na kwa vipi inawezekana kukaa ndani yake? Kukaa katika pendo lake? Na je tunaweza kupanda mbegu hiyo katika   familia zetu, katika sehemu za kazi zetu na  katika jumuiya zetu, kupanda mbegu ile ya  umoja ambao  Yeye aliutoa kwetu  kama  washarika katika maisha ya Utatu?
Kwa maswali hayo, Papa alikamilisha homilia yake , na wito kwa wote kudumu na furaha hii kukutana  na Bwana Mfufuka katika maisha na kupandikiza  kama wajibu , moyo  wenye shikamana na upendo wa Mungu .  Kubaki katika umoja na Mungu, na kati yetu wenyewe, na kufuata nyayo za wanawake hawa wanne, mifano ya utakatifu ambao Kanisa linatualika kuiga.

Papa aliikumbuka pia Burundi 

Baada ya maadhimisho haya, wakati wa sala ya Malaika wa Bwana, Papa kwa namna ya kipekee wakati akitoa salaam zake kwa makundi mbalimbali ya watu wote waliofika kutoa heshima zao kwa Watakatifu mpya, alilikumbuka taifa la Burundi ambako kwa wakti huu linateswa na hali teke za kisiasa. Alonyesh akujali mateso ya watu wengi Burundi hasa wanaolazimika kuondoka katika makazi yao, kama hatu ayakusalimisha maisha yao. Na hivyo akatoa mwaliko kwa watu wote, kuwaombea wakimbizi na hasa wanasiasa na viongozi waweze kuona umuhimu wa kazi yao na huduma yao iwe ni k wa manufaa ya taifa zima la Burundi na si kwa manufaa yao binafsi.  

Katika salaam hizo Papa pia aliugeukia pia makundi makubwa ya waamini waliotoka Palestina, Ufaransa, Italia, Israel na Jordan kwa ajili ya tukio la Ibada hii. Na pia aliwasalimia kwa upendo mkuu  Makardinali, Maaskofu, mapadre na Watawa  mabinti wa kiroho wa Watakatifu wanne wapya. Papa alisali ili kupitia maombezi ya Watakatifu wapya Bwana ruzuku, aweze kutoa  msukumo mpya wa kimisionari kwa nchi zao ya asilia. Maisha ya Watakatifu wapya yaweze kuongoza katika njia ya maisha  mtu kuwa mwenye huruma, upendo na maridhiano. Na  Wakristo wa nchi zao waweze  kujazwa na matumaini kwa   siku za usoni,wakiendelea kutembea katika mwelekeo wa mshikamano, umoja na udugu.

Aidha Papa alipeleka salaam zake kwa familia, vikundi kanisa, vyama na shule tokea Jimbo Kuu ya Genoa, na pia kwa waamini wa  Jamhuri ya Czech, ambao wamefanya kumbukumbu ya kupita miaka  ishirini ya ziara ya Mtakatifu Yohana Paulo  II. Na pia alikumbuka tukio la Jumamosi la kutangazwa kuwa Mwenye Heri Don Luigi  kwa Caburlotto, mchungaji, mwalimu na muasisi wa Shirika la Masista Mabinti wa Mtakatifu  Joseph. Namshukuru Mungu kwa hili Mchungaji mfano, ambaye aliongoza kiroho na ya kitume maisha makali, kujitolea kabisa kwa faida ya nafsi.  Kwa upendo usiotenganisha aliwataka wote kutolea sala kwa  Bikira Maria, Mama wa Kanisa, Malkia wa Watakatifu na mfano wa Wakristo wote.








All the contents on this site are copyrighted ©.