2015-05-16 14:11:00

Msimamo Katoliki wa Malta juu ya upandikizaji viungo vya mwili


Baraza la Maaskofu Katoliki katika Jamhuri ya Kisiwa Malta, limetoa tamko lake la kichungaji juu ya utaalam wa kupandikiza viungo vya mwili kwa wahitaji, na onyo kwamba, kamwe huduma hiyo isiwe uwanja wa biashara ya viungo.  Msimamo wa Maaskofu, umo katika hati ya Kichungaji ya Maaskofu iliyowasilishwa katika mkutano wa  pamoja wa viongozi wa dini na wataalamu katika uwanja wa dawa na tiba,  wanasaikolojia, wanafalsafa na wanateolojia.Mkutano ulioitikia wito wa Serikali, na wadau wote wa kijamii , kutoa maoni yao katika vipengere muhimu vinayohusika na maendeleo na uundaji wa sera ya afya , hasa kwa ajili ya upandikizaji wa viungo vya mwili kwa wahitaji.

Hati ya  Kichungaji ya Maaskofu ilitoa msimamo wake katika vipengere kadhaa, ikianza na  Sera sasa, juu ya upandikizaji wa viungo na vikonyo vya chembe hai, ikilinganisha na maamuzi ya nchi nyingine wanachama wa Umoja wa Ulaya.  Kwa mujibu wa utafiti wa hivi karibuni, Malta inashika nafasi ya pili katika utoaji wa viungo . Aidha, takwimu zinaonyesha kwamba mfumo wa sasa  unafanya kazi  vizuri na hutoa msingi wa utendaji unaofaa kwa ajili ya maendeleo zaidi  juu ya huduma hii. Hivyo Maaskofu wa Malta wameshauri , sheria yo yote mpya juu ya huduma hii iwe ni  kuboresha badala ya kubadili mfumo wa sasa.

Pili Maaskofu wamehimiza kwamba, uamuzi wa mtu kuchangia viungo au kiungo kwa ajili ya kusaidia mhitaji , iwe ni kitendo cha huruma upendo na  ukarimu na si kamwe isifanyike katika mfumo wa kibiashara.  Mtu hawezi kupokea kama zawadi kutoka kwa wengine, iwapo zawadi hiyo haitolewi kwa moyo wa hiari na uhuru kamili. Zawadi ni kitu kinachotolewa kwa  ridhaa ya bure,  na si utoaji ni nipe  nikupe, au katika mitazamo ya kuzalisha faida. Kutafuta faida ni kuwa kinyume na maadili.Hati hiyo imekumbusha kwamba, tangu mafanikio ya kwanza ya tiba ya  kupandikiza viungo katika miaka ya hamsini mwanzoni, Kanisa Katoliki limesaidia kutoa mchango wake wazi unaounga mkono huduma hii kutoka kwa aidha kwa mtu aliye hai au kutoka kwa Marehemu , lakini daima katika msisitizo kwamba, ni lazima viungo vitolewe katika mazingira ya kweli ya haki na kanuni ya upendo na mshikamano.

Tatu mchango wa Maaskofu umekazia masuala ya Maadili, kwamba, ni lazima dhana ya umiliki wote wa viungo ibaki kuwa  ni maamuzi binafsi yasiyolazimika kuwa na sheria mbadala katika mifumo ya sera za kiserikali , kwa kuwa mwili wa mtu, ni binafsi, ambao hauwezi kutegemea maamuzi ya kisemrikali , lakini basi iwapo unatolewa kwa manufaa ya wengine linakuwa ni jamb o binafsi linalopokelewa kamazawadi kwa wengine na si shuruti . Kwa maana hiyo viungo vyote vinavyotolewa kwa sababu za uadilifu si kitu cha kufanyiwa biashara.  

Maaskofu wameeleza katika hati yao ya kichungaji huku wakionyesha kujali kwamba, Mfumo mbadala  unaweza haribu haribu asili ya mchango wa zawadi hiiya kiungo inayotolewa kama zawadi  kwa mtu muhitaji. Na hivyo kuondokana na kujenga hofu katika akili za watu juu hili, ni vyema kuhakikisha serikali inachukua hatua zinazofaa katika haki miliki ya viungo na mwili wa kila mtu.  Na hivyo  uvunaji wa viungo kutoka watoto wanaozaliwa, si hoja inayoibua uwajibikaji mkali wa  kimaadili..

Mwisho Maaskofu walikamilisha kwa kutoa mapendekezo yao kwamba, dhana ya utoaji wa viungo , ni lazima iwe katika mtazamo wa zawadi ya hiari, kama jambo linalotakia kulindwa na kudumishwa. Hivyo, sheria mpya lazima ziimarishwe  katika mtazamo huo.  Hati inatoa msimamo  huo thabiti kwa ajili ya hatua zote zitakazojalidiliwa kwa lengo la kutaka  kuboresha  mfumo mbadala, au usimamizi wa Maoni kwa ufanisi zaidi au marekebisho zaidi .








All the contents on this site are copyrighted ©.