2015-05-13 10:48:00

Naomba, Asante, Nisamehe, maneno yanayojenga msingi imara wa familia


Baba Mtakatifu katika Katekesi yake ya kila Jumatano, ameendelea na Mada juu ya familia , leo akitafakari juu ya maneno matatu ya kawaida  “Naomba”,  "Asante", na "nisamehe ". Alianza kusema , maneno haya kawaida, kwa leo hii yanaonekana si rahisi kutamkwa  na hasa  kimatendo.  Lakini wakati yanapopuuzwa , na kukosekana kwake katika  mazungumzo ya kila siku ndani ya familia, husababisha nyufa myimgi katika msingi wa maisha ya familia, na hivyo kunaweza leta uharibifu mkubwahata familia kusambaratika.   Lakini iwapo maneno haya yanakuwa ni  sehemu ya maisha yetu ya kila siku, sio tu yanakuwa usemi rasmi wenye kuonyesha  tabia njema, lakini pia kama ishara ya upendo kina kwa ajili ya mtu mwingine, ni maneno yenye kuimarisha maisha ya familia na furaha.

Papa aliendelea kufafanua kwa kina , neno “naomba “hata kama ni haki kupata jambo hilo,  wakati tunapozungumza na  wenzi wetu au familia zetu  kwa upole na unyenyekevu ,mnakuwa na nguvu ya kutengeneza nafasi kwa ajili ya roho ya ukweli katika  maisha ya kawaida , hasa maisha ya  ndoa na familia.  Neno hili "naomba " pia peke yake huonyesha upya   imani na heshima, kwa wengine na huruhusu  kufungua mlango wa moyo wetu kwa wengine. 

Papa aliendelea na Neno  "Asante" akisema,  kuna haja kubwa kwa  jamii yetu kuwa na moyo wa shukrani,   kutoa shukurani hizo kwa neno moja tu "asante ", neno linalotufanya sisi kuona unyeti  wa hadhi ya binadamu na mahitaji ya haki za kijamii.  Shukrani pia ni lugha ya Mungu, ambaye zaidi ya yote,sisi  sote ni  lazima tunapaswa kusema Asante kwake kwa mengi mema anayotujalia bila hata kumwomba.

Papa aliendelea na neno "Nisamehe” akisema  bila uwepo wake huweza umiza maendeleo  katika uhusiano , hivyo  kudhoofisha maisha yetu kama familia. Kwa kuomba  msamaha,  huonyesha hamu ya kutaka kurejesha upya kile kilichopotea katika uhusiano wetu,  heshima, uaminifu na upendo.  Nisamehe ni neno la uponyaji kati ya wanafamilia na lina uwezo wa kufanya hivyo.

Baba Mtakatifu alimalizia mafundisho kwa kumwomba Bwana atuwezeshe  kuyaweka moyoni maneno haya "Naomba", "Asante", "Nisamehei"ndani ya mioyo yetu, katika familia zetu na  jamii zetu.

Baada ya Katekesi  Papa alisalimia kwa moyo wa dhati makundi ya mahujaji na wageni waliofika kumsikiliza na wengi wao wakiwa kutoka Uingereza, Sweden, Taiwan, Cameroon na Marekani.   Aliwatakia nguvu ya Kristo iweze kuwaimarisha zaidi na zaidi imani yao na imani kwa familia zao , ili daima ulimwengu uweze ona upendo wa Mungu na huruma yake.
 








All the contents on this site are copyrighted ©.