2015-05-04 14:20:00

Kusalimisha mazingira asilia Afrika ni lazima uwepo wa ushirikiano wa kimataifa


Mkutano wa siku tatu wa Wakuu wa Nchi katika Kanda Maziwa Makuu na watoa maamuzi wengine , ulifanyika kwa ufadhili wa Rais wa  Jamhuri ya Congo Brazzavile, tangu tarehe 27-30 Aprili 2015, kwa ajili kupambana na  Biashara haramu ya wanyama pori na mimea  wanaoporwa toka barani Afrika. Mkutano huu ni mwendelezo wa juhudi zinazolenga kusalimisha uwepo wa aina zote za wanyama na mimea asilia barani Afrika. Mkutano ulibaini kwamba usafirishaji wa wanyamapori  unaendelea kuwepo kutokana na  uhaba wa  vyombo vya ulinzi thabiti,ikishamirishwa na uwepo wa migogoro ya kisiasa  na rushwa. Pamoja na ujangili  huo pia kuna uchimbaji haramu wa madini unaonyonya utajiri wa Afrika bila kunufaisha wenyeji , kutokana na udhaifu katika utekelezaji wa  sheria  za serikali, wenye kuruhusu mgawanyiko katika  jamii.

Wajumbe  katika mkutano wao walisisitiza kwamba, jamii inapaswa kuwa na ufahamu wa kutosha , juu ya madhara ya  usafirishaji haramu wa Wanyamapori,  pia kwamba , ni  kuharibu viumbe hai na mazingira, na ni tishio katika  upatikanaji wa chakula na maji safi na humomonyoa  maisha ya mamilioni ya watu barani Afrika.

Mkutano huu wa hivi karibuni uliandaliwa na Serikali ya Jamhuri ya Congo na Tume ya Umoja wa Afrika (AUC), kwa kushirikiana na UNEP na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP). Baada ya mkutano huu kinachofuata ni Mkutano mwingine wa 23 wa Umoja wa Afrika , unalenga kutoa wito kwa mataifa ya Afrika , kutumia uwezo na mbinu thabiti, katika  kuchukua hatua za kuimarisha sheria na sera, na ushirikiano na jamii, kwa ajili ya kupambana na biashara haramu ya wanyamapori na shughuli zinazohusiana na uhalifu huo. Mkutano unalenga  kujaribu kujenga mkakati  wa Afrika nzima, ikihusishwa na mpango wa utekelezaji  dhidi ya biashara haramu ya wanyama pori na mimea, mapendekezo yatakayo fikishwa katika Mkutano ujao wa  AU, kwa ajili ya maamuzi zaidi ya utekelezaji.

Kati ya viongozi wakuu walioshiriki katika Mkutano wa Kimataifa wa 27-03 Aprili 2015,  juu ya Biashara haramu ya  pori wanyama na mimea, uliofanyika katika Ikulu ya Congo Brazzaville ni pamoja na mwenyeji wa mkutano  Rais Denis Sassou Nguesso, pia Marais na Wakuu wa Nchi kutoka Mkoa wa Maziwa Makuu waliokuwa wameandamana na  , Waheshimiwa Mawaziri  wa Wizara zinazohusika na  Wanyamapori,  pia akiwepo Kamishna wa Uchumi wa Vijiji  na Kilimo wa AU,  na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa UNEP, na Mratibu Mkazi wa UN na UNDP, Mwakilishi Mkazi nchini Kongo.

Katika Mkutano huu , wajumbe walihimiza zaidi uratibu mzuri  wa vyombo vya upelelezi,  na utekelezaji wa sheria, wenye kuishirikisha jamii yote ya  Afrika kwa kushirikiana na serikali za nchi ambako  bidhaa  zina soko. Wote kwa pamoja ni lazima kuwa kujenga moyo thabiti katika kuikataa biashara hii ya kutisha  na  kukabiliana nayo. Nchi lazima zilichukue kama dharura, inayo hitaji uratibu wa karibu wa kimataifa, ktika kukomesha  ujangili na uporaji wa mali za Afrika. Ni kuwa na udhibiti mkali wa polisi, ikiwa ni pamoja na kuimarisha ukaguzi katika maeneo ya mpakani.

Rais Nguesso ameitaka  jumuiya ya kimataifa ili kuendeleza  ushirikiano wake katika  hili na hasa uhamasishaji  dhidi ya uhalifu wa mazingira na kufanya imara sheria zinazowekwa na nchi kwa ajili ya apambano dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi na changamoto nyingine duniani. Na kwamba hakuna nchi inayoweza kufanikiwa katika mapambano haya bila ushirikiano wa kimataifa. 








All the contents on this site are copyrighted ©.