2015-04-18 13:50:00

Uhusiano wa karibu kati ya Italia na Vatican ni matunda ya kuheshimiana


Na Rais wa Italia , Sergio Matterella,  akimtembelea Papa Francisko mjini Vatican mapema Jumamosi hii, katika hotuba yake, ameonyesha shukurani zake za dhati kwa Papa Francisco kwa ushuhuda wake wa thamani, wenye kuonyesha uhusiano maalum na wa kipekee kati ya  Kiti Kitakatifu  na Jamhuri ya Italia..Hivyo Rais Sergio, kwa niaba yake mwenyewe na kwa niaba ya Wananchi wa Italia ,alipenda kufikisha salaam za upendo, urafiki  katika  mahusiano haya  yenye mwelekeo wa kukua siku baada ya siku. 

Pia Rais ameshukuru  kwa maneno ya matumaini yaliyotolewa  Papa Francisko kwamba yatasaidia  kuokoa thamani ya mshikamano na umoja wa watu wa Italia, katika mazingira ya nyakati hizi, zilizojaa  wasiwasi na mashaka , kwenye  wigo wa hisia za watu, hasa katika nyakati za mgogoro na shida.  Na ameutaja uhusiano wa karibu kati ya Italia na Nchi ya Jiji la  Vatican,  kuwa  umesimikwa katika  mizizi na  sura ya kipekee ya  kihistoria,  kama ujirani mwema kati ya mataifa haya mawili. Uhusiano unaoenezwa na kuendelezwa kwa njia ya kuheshimiana. Na pia alishukuru  Mafundisho Papa, yenye kulenga  moja kwa moja katika  ukweli wote na  hata  juu ya masuala ya kijamii, kiuchumi na kisiasa ya Italia. Rais Mattarella alieleza na kurejea nyaraka mbalimbali za Kitume za Mapapa , zenye kuwa na utajiri wa maadili katikia kazi za kukuza, amani, maendeleo na , heshima ya binadamu.

Aidha Rais  Matterella ,amerejea utendaji mbalimbali wa Papa Francisco, akitaja tangu  ziara yake ya kwanza ya  kichungaji nchini Italia katika  eneo la Lampedusa, na ile aliyoifanyika hivi karibuni,  Naples, ambamo katika zote alionyesha mshikamano wake katika kujali matatizo na matarajio ya Italia. Rais ameonyesha matumaini yake katika  Jubilee ya Huruma ya Mungu aliyoitangaza Papa Francisko hivi karibuni kwamba,  itatoa nafasi ya kutafakari  juu ya thamani ya maadili ya haki na mshikamano wa kweli na maana ya kuwa na amani. Ameonyesha kutambua kwamba , katika wakati wetu huu  mienendo ya kiuchumi mara nyingi  inapoteza  mwelekeo wa ubinadamu, na hivyo kujenga kitisho cha kuendeleza dhuluma, zenye kuishia katika  migogoro na ukosefu wa  usalama. Na hivyo  wito wa kutafuta Huruma ya Mungu, unaweza kufufua upya  miongoni mwa watu, maisha mapya yenye kuona  thamani  ya mahusiano mazuri ya kiuchumi na kijamii kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya wote.

Na kwamba,  Uhuru wa kidini ni ya matarajio halisi  na msingi yaliyomo katika Katiba ya Italia. Ukiukaji  wowote ule, inakuwa ni kuvunja  haki za binadamu na jamii. Na hivyo vurugu zozote zinazofanywa dhidi ya jamii ya Kikristo katika baadhi ya maeneo,  inakuwa ni  changamoto dunia, inayohitaji kutafutiwa  jibu la nguvu la pamoja  katika dhamiri za wote wanaopenda  uhuru na kuvumiliana.  Italia anahisi nia, na mshikamano wa kimataifa kupambana na ugaidi , kuwa sehemu ya jumuiya ya kimataifa, kwa sababu ni utendaji  wenye kuzingatia  kanuni za maelewano na ushirikiano, sharti msingi kwa ajili ya amani ya kweli.

Rais Mattarella alikamilisha hotuba yake kwa kurudia kutoa upya mwaliko kwa Papa Francisko, aitembelee tena Ikulu ya Italia, kwa ajili ya kuimarisha zaidi mazungumzo yao, na kwa ajili ya  mwendelezo wa mahusiano haya  maalum yanayosindikiza uhusiano thabiti kati ya Kiti Kitakatifu na Jamhuri ya Italia. 








All the contents on this site are copyrighted ©.