2015-04-05 13:49:00

Mkesha wa Pasaka maana yake ni kuingia katika Fumbo la wokovu


Homilia ya Baba Mtakatifu Francisko kwa wakati wa Mkesha wa Papa,  ilianza na tafakari juu ya tukio lenyewe akisema , katika  usiku huu wa mkesha, Bwana hatasinzia wala hatalala, ni mlinzi kwa watu wake,  hadi atakapowatoa katika  utumwa , akiiweka  wazi mbele yao  njia  ya uhuru. Papa aliongoza Ibada ya Mkesha wa Pasaka , katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, Usiku wa Jumamosi Kuu.

Papa aliuzungumzia Usiku huu Mkuu , ambamo Bwana anakesha na kwa nguvu ya upendo wake , anawapitisha watu wake katika Bahari ya Shamu, na ndivyo anavyomleta Yesu  kupitia njia ya dimbwi la kifo na dunia ya kuzimu.

Huu ulikuwa ni usiku wa mkesha kwa wanafunzi wa Yesu,  usiku wa uchungu na hofu kuu.  Wanaume walibaki wamejifungia katika chumba cha Juu . Lakini wanawake   alfajiri ya baada ya Sabato, walienda kaburini, kwa nia ya kutaka kuupaka mafuta mwili wa Yesu. Mioyo yao ilijaa mashaka , wakijiuliza maswali mengi, watawezaje kuingia ndani ,  nani atakaye waondolea lile jiwe la  mlangoni pa kaburi? ...  Lakini mara walipata  ishara ya kwanza ya  kuingia ndani,  jiwe kubwa  walilokuwa wakilihofia , lilikuwa  tayari limeviringishwa mbali na kaburi hilo. Kaburi  lilikuwa wazi!

Na walipoingia kaburini walimwona kijana ameketi upande wa kulia, aliyevaa vazi jeupe ..." (Mk 16.5). Hivyo wanawake walikuwa wa kwanza kuona ishara hii kubwa: kaburi tupu, na walikuwa wa kwanza kuingia ...
 

Baba Mtakatifu alifafanua  kiliturujia  maana ya  kuingia ndani ya kaburi, akisema  kuwa ni jambo jema wakati wa Mkesha huu, kupata  uzoefu wa wanawake hao . Na hiyo ndiyo ilikuwa maana ya  kushiriki kaika Ibada  ya Mkesha wa Pasaka. Maana yake ni kuingia ndani ya fumbo, ambamo Mungu anakamilisha kazi yake ulinzi kwa upendo.  Na hatuwezi kuwa na Pasaka bila ya kuingia katika fumbo hili.  Si kwa  ujanja wa  akili, au jambo tunalolifahamu au kulisoma habari zake , lakini ni zaidi ya hayo, ni mengi zaidi!

Na kwamba , kuingia katika fumbo hili,  maana yake ni kuwa na uwezo wa kuona maajabu haya , ni kuwa na uwezo wa kusikiliza ukimya  na ming’ong’no midogo kati ya ukimya ambamo Mungu anazungumza nasi (cf. 1 Wafalme 19:12).


Kuingia katika fumbo hili , kunatutaka kutohofia hali halisi. Ina maana  tusibaki tumejifungia  katika dhambi zetu  na mambo tuliyozoea , tusijifungie ndani mwetu , na wala si kuyakimbia yale tusiyoyaelewa , na si kufumbia macho matatizo ya wengine  au kukanusha au kuyafuta  maswali ... Bali kuingia katika fumbo huili ina maana ya kuyashiriki pia matatizo ya wenzetu , tukijikatalia  hali nzuri za maisha yetu ,ni kuuweka  uzembe na tofauti zinazoturudisha  nyuma , katika mwendo ni kusonga mbele  kuutafuta ukweli, uzuri na upendo wa Mungu.  Ni kutafuta maana ya kina ya  jibu,  ambalo si la kijuujuu  katika  hoja zinazokuwa changamoto kwa imani yetu, uaminifu wetu na uhalisi wetu.

 Kuingia katika fumbo hili, tunahitaji unyenyekevu, kuushusha ufahari wetu  binafsi, kushuka toka kinara cha mimi na  dhania zetu , na kuwa na  unyenyekevu  wa  kutojiona wa maana kuliko wengine, ni kutambua hadhi yetu kwamba ,  ni  viumbe wenye dhaifu, wenye dhambi  wanaohitaji  msamaha. Kuingia katika fumbo  hili inahitaji kujishusha kijasiri , katika kukataa  uovu  tunayopenda kuabudu. .

Papa  Francisco aliendelea kusema, Wanawake  wa kwanza, wafuasi  wa Yesu wanatufundisha sisi yote hayo. Katika Usiku wa Jumamosi Kuu , waliukesha usiku ule wakiwa na Maria. Na Bikira Maria aliwasaidia kutopoteza imani na tumaini. Kama matokeo yake , hawakubaki kama wafungwa wa hofu na huzuni ,maana  mara mwanga wa siku ulivyotokea , walichukua  mikononi  mwao, marhamu,  mioyo yao ikiwa imepakwa mafuta ya upendo. Walikwenda na kukuta kaburi li wazi na kuingia ndani  ya fumbo la Pasaka. Hili linatufundisha  sisi kukesha na Mungu, tukiwa karibu na Mama yetu Maria , ili pia sisi tuweze kuingia katika fumbo hili la kutoka katika kifo hadi maisha.

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.