Kila Mwaka tarehe 25 Machi, Umoja wa Mataifa unaadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kumbukumbu ya Waathirika wa Utumwa na biashara ya utumwa kupitia Bahari ya Atlantiki Siku hii hutoa nafasi kwa watu wote kuheshimu, kuomboleza na kuwakumbuka wale wote walioteseka na kufa chini ya mfumo katili wa utumwa. Siku hii inalenga kuhamasisha watu wafahamu na pia kushiriki katika kutokomeza aina zote za utumwa, ubaguzi wa rangi na dharau zinazojitokeza leo hii.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni, “Wanawake na Utumwa”. Kauli mbiu hii inawaenzi wanawake
wote watumwa waliovumilia mateso makali yakiwemo mateso ya kutumika vibaya kingono
pamoja na kuwaenzi wanawake wote waliopigania uhuru kutoka utumwani na waliohakikisha
utumwa unafutwa. Vilevile kauli mbiu hii inawasherehekea wanawake wote waliokuwa watumwa
na ambao walifanikiwa kuwarithisha wanao jadi na tamaduni zao licha ya shinikizo mbalimbali
na ukatili waliokuwa wakipitia.
Duniani kote kutakuwa na maadhimisho mbalimbali ikiwemo kusimikwa kwa ‘Sanduku la
Mrejeo’ yaani Ark of return katika Makao makuu ya Umoja wa Mataifa. Hili Sanduku la
mrejeo limetengenezwa na Rodney Leon ambaye ni msanifu wa Marekani kutoka Haiti. Ni
chombo ambacho kimesimikwa kama kumbukumbu ya kutambua kuwa mamilioni ya watu wa Afrika
walisafirishwa katika mazingira magumu. Wageni watapaswa kuingia katika sanduku la
mrejeo ili kupata kwa undani uzoefu wa mambo matatu makubwa: kutambua uwepo wa janga
hilo, kutafakatri kumbukumbu iliyobaki na kutosahau asilani.
All the contents on this site are copyrighted ©. |