Baba Mtakatifu Francisko, katika kipindi hiki cha Kwaresima, amewaandikia barua
ndugu zake Maaskofu Katoliki wa Nigeria, ambamo ameomba pia wafikishe salaam zake
kwa Jumuiya za Kikristo walizopewa dhamana katika huduma za kichungaji. Papa ameonyesha
mshikamano na mawazo yake juu ya hali ngumu wanazopita, kwa wakati huu.
Habari kamili
Katika barua hiyo, Papa amesema, “wakati huu tunapotembea kuelekea ufufuko wa Bwana
tukiwa tumeungana pamoja na kanisa zima, ninapenda kutoa saalam zangu za dhati ,
kwenu nyote Maaskofu Wakuu na Maaskofu wa Nigeria , na pia nikiwaomba zifikishe kwa
jamii Kikristo mliyokabidhiwa katika huduma ya kichungaji. Aidha ninapenda kushirikishana
nanyi , baadhi ya mawazo yangu kuhusu hali halisi za sasa za maisha katika nchi
yenu”.
Barua ya Papa , imeendelea kuielezea katika mtazamo wa maisha ya kijamii taifa hili
la igeria, taifa kubwa kuliko yote barani Afrika , lenye kuwa na raia zaidi ya milioni
160, linalojulikana pia kwa utendaji wake si barani Afrika tu lakini duniani kote.
Ameonyesha kutambua jinsi taifa hilo katika miaka ya hivi karibuni limeweza kushuhudia
ukuaji wa haraka wa uchumi na pia kwa mara nyingine kujiwasilisha katika jukwaa la
kimataifa kama soko la kuvutia , kutokana na uwepo wa rasilimali nyingi, na kwa
uwezo wake wa kibiashara. Na pia kwa jinsi linavyojitambulisha lenyewe kuwa mtendaji
mkuu katika utatuzi wa baadhi ya migogoro ya kisiasa barani Afrika.
Lakini wakati huohuo, barua ya Papa imeonyesha kujali matatizo makubwa yanayo kabili
taifa hilo , ikiwa ni pamoja na aina mpya ya vurugu za kuvuka mipaka na misimamo mkali
inayoendeshwa kikabila, kijamii na kidini, ambamo kwayo Wanigeria wengi wameuawa,
kujeruhiwa na kuwa vilema, kutekwa na kupokonywa kila vitu au si mali tu lakini hata
wapendwa wao, nchi yao, maisha yao , utu wao na haki zao, kiasi kwamba watu wengi
hawawezi kurudi makwao. Wote sawia Waumini, Wakristo na Waislamu, wanayapita mateso
haya makubwa kama matokeo ya wachache wanaodai kuwa watu wa dini zaidi , ambao hulitumia
jina la dini vibaya kwa kutengeneza itikadi zao za kidini kwa maslahi yao kupitia
ukandamizaji na vitisho vya kifo.
Katika hali hizo, Papa alipenda kuwahakikishia kwamba yu karibu na Maaskofu na wale
wote wanaoishi mateso na unyanyasaji huo . Na kwamba kila siku anawakumbuka katika
sala zake nakwa mara nyingie anapenda kuwatia shime na faraja kwa maneno ya kufariji
ya Yesu Kristo, yanayopaswa kusikika daima ndani y amoyo wa kila mmoja :"Nawaachieni
amani, amani yangu nawapa" (Yoh 14:27).
Amani, Papa ameendelea kusema, si tu kutokuwepo vita au kuwa na maelewano katika
baadhi ya vipengere vya kisiasa, au kutokuwa na ubabe wa kupindukia. Lakini watu
wanapaswa kutambua kwamba amani, ni kwa ajili wote, kama zawadi inayotoka kwa Yesu
Kristo , Mfalme wa amani, anayewafanya wawili kuwa sawa na mtu mmoja Efe. 2:14). Lakini
ameonya kwamba, ni tu wale wenye kupokea amani ya Kristo ndani ya mioyo yao
na kuihifadhi, kama mwanga wa kuwaongoza katika njia ya maisha, wanaweza kuwa wajenzi
wa amani (Rej. Mt 5,9.).
Na kwamba amani ni utendaji wa kila siku, ni kuwa na ujasiri katika kuiishi halisi
ya kukuza maridhiano na ushirikiano kame sehemu ya uzoefu wa maisha, na kupanua ujenzi
wa madaraja ya majadiliano, huduma kwa wanaoishi kwenye mazingira magumu na wanyonge
zaidi waliotengwa. Kwa maneno mengine, amani ni ujenzi wa utamaduni wa kukutana.
Katika Barua hii, Papa pia alipenda kutoa shukurani zake za dhati kwa Maaskofu,
kwa sababu katikati ya majaribu mengi na mateso, Kanisa nchini Nigeria, limeendelea
kuhudumia kwa ukarimu, huruma na msamaha. Na hivyo amewakumbuka Mapadre, watawa wake
kwa waume, wamisionari na makatekista ambao licha ya kuhatarisha maisha yao, hatelekezi
watu wao wanao waongoza bali huendelea kubaki imara katika utumishi wao, wakihubiri
wema na uaminifu wa Injili.
Kwao wote , Papa ametoa shukurani zake za dhati na kuonyesha mshikamano wake , na
kuwataka wasichoke kutenda mema. Kwa ajili yao alitolea shukurani kwa Bwana pia kwa
watu wengi toka pande mbalimbali za kijamii, kiutamaduni na kidini ambao kwa mapenzi
yao na maamuzi yao thabiti, wamesimama imara kupinga kila aina ya ghasia na fujo ,
na kwa wale wote wenye kupendelea neema ya usalama na utulivu kwa ajili ya wote.
Papa amewataja watu hao kuwa ni mfano mzuri wenye kutia nguvu mpya ya kusonga
mbele katika kushuhudia manufaa ya amani kama Papa Mstaafu Benedikto wa XVI, alivyoandika
katika waraka wa mwisho wa Sinodi kwa ajili ya Afrika, kwamba, amani ni matokeo ya
utendaji wa nguvu ya Roho Mtakatifu ambayo hubadilisha mioyo ya waathirika na watesaji
wao na hivyo kuweza kurejesha udugu" (Africae Munus, 20) .
Kwa maono haya Papa Francisko amewahimiza ndugu zake Maaskofu wa Nigeria, kudumu katika uvumilivu na bila kukata tamaa, bali wasonga mbele pamoja katika njia ya amani (rej Lk 1:79.)na katika kuwaongoza waathirika, kusaidia maskini na kuelimisha vijana ili kwamba wote wawe wakuzaji wa haki na umoja katika jamii ya Nigeria. .
Mwisho Papa, kupitia barua hii kwa Maaskofu , ametoa baraka zake za Kitume, pia Mapadre, watawa, wamisionari, makatekista, waamini na wale wanaotesekana kwa imani yao kwa Kristo . Amesema Ufufuo wa Bwana na uwe kichocheo cha uongofu, maridhiano na amani kwa watu wote wa Nigeria! Na mwisho kabisa amewakabidhi chini ya maombezi ya Mama Maria, Malkia wa Afrika. Na ameomba wasimsahau katika sala zao. .
All the contents on this site are copyrighted ©. |