2015-02-24 13:55:48

Mapinduzi kijani: Afrika yahitaji teknolojia mpya


Bara la Afrika limeonywa dhidi ya kuiga kipofu, majawabu ya mabara mengine katika kutatua matatizo ya Afrika. Onyo hilo, limetolewa na watafiti wa Kimataifa wa Taasisi ya Sera ya Chakula na Utafiti, IFPRI.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari inasema, nchi za Kiafrika zisiige kiholela au kupitisha mikakati ya sera ya chakula kipofu, katika lengo lake la kufanikisha mapinduzi ya kijani. NI lazima mikakati ya utekelezaji ilenge katika hali halisi za matatizo mahalia ya Afrika. IFPRI, imetoa ushauri huo, kwa kuzingatia matokea ya utafiti wake uliofanyika nchini Ghana.

Matokeo ya awali yaliyochapishwa katika jarida Sera ya Chakula, yalionyesha kwamba, Afrika badala ya kulenga tu katika uzalishaji wa chakula, ni lazima kuwa na mbadala wa kuendeleza teknolojia mpya, katika kuboresha pia pato la miti na mazao ya mizizi, ambayo hupatikana kwa wingi katika kanda ya Afrika, na pia kama njia ya kupunguza uzito wa kazi za mikono kwa wananchi wa Afrika.

Matokeo ya utafiti huo yameanisha, Mapinduzi ya Kijani ya miaka ya 1960 na 1970, katika nchi za Asia na Amerika ya Kusini, zilizo weza kufanikisha ongezeko kubwa katika uzalishaji wa ngano na mazao mengine ya chakula, kwa kutumia mbinu mpya za kilimo na hasa zaidi kuongeza matumizi ya mbolea na kilimo cha umwagiliaji. Nchi za Afrika pamoja na kuwa na hamu ya kuiga mafanikio hayo, na kupitishwa sera zinazofanana, hazijafanikiwa kuongeza mazao ya kilimo.

Mtafiti Mkuu wa IFPRI, Alejandro Nin-Pratt, katika taarifa hiyo anaonya Afrika, isifanye kosa jingine la kuiga kiholela mtindo uliofanikisha kuleta mapinduzi kijani barani Asia , na hivyo kuepuka kukatishwa tamaa iwapo malengo yatashindwa kufanikiwa kama inavyotazamiwa kufikia ukuaji endelevu katika kilimo.

Hapo Februari 19, Nin-Pratt alipokea tuzo ya Elsevier Atlas, kwa kazi yake ya kina, katika kuona sababu zinazoweza kufanikisha muafaka kwa Mapinduzi ya Kijani kwa nchi za Afrika. Tuzo Atlas hutoa hutolewa kama kuheshimu kazi kubwa iliyofanywa na watafiti katika kutoa mchango mkubwa katika kufanikisha maendeleo ya binadamu kwa njia ya sayansi.

Utafiti wa Nin-Pratt, ulilenga kwa wakulima wadogowadogo nchini Ghana, ambao hutumia mbolea kidogo, wakichukuliwa kama mfano kwa mataifa mengine ya Afrika . Ghana ilichaguliwa kwa ajili ya utafiti kutokana na uwezo wake katika ukuaji wa haraka wa idadi ya watu na utendaji a kuonekana katika mabadiliko ya kilimo. Imeonekana kasi ya ongezeko la watu Afrika, haina matokeo ya kupunguza gharama za nguvu kazi katika kazi za kilimo.








All the contents on this site are copyrighted ©.