Baba Mtakatifu Francisko wakati wa hija yake ya kitume nchini Sri Lanka, Familia ya
Mungu, Jimbo kuu la Colombo, lilimpatia zaidi ya Millioni 8. 7 fedha ya Sri Lanka
ili kuchangia mfuko wa mshikamano wa upendo unaotekelezwa na Baba Mtakatifu Francisko.
Hivi karibuni, Baba Mtakatifu Francisko amemrudishia fedha hii ambayo ni sawa na Euro
zaidi ya 57, 000 Kardinali Malcolm Ranjith, ili zichangie huduma kwa maskini na wote
wanaosukumizwa pembezoni mwa jamii nchini Sri Lanka.
Ukarimu huu ulimgusa sana
Baba Mtakatifu Francisko kiasi cha kusema kwamba, hata maskini katika umaskini wao
ni wadau wakuu wa Uinjilishaji kwa njia ya ushuhuda wa maisha. Baba Mtakatifu anamwomba
Kardinali Ranjith kumpatia maelezo ya kina jinsi fedha kwa ajili ya kuwasaidia maskini
ilivyotumika.
Taarifa zinaonesha kwamba, fedha hii imegawanywa kwenye Majimbo
mbali mbali nchini Sri Lanka ili kuwasaidia maskini kama changamoto ya ujenzi wa mshikamano
wa utandawazi unaojali na kuguswa na mahangaiko ya wengine.
Na Padre Richard
A. Mjigwa, C.PP.S. Idhaa ya Kiswahili ya radio Vatican.