Baba Mwalunyungu, kapumzike kwa amani, kazi ulifanya!
Waziri mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda amewataka Watanzania wasikilize na kufuatamafundisho
yanayotolewa na viongozi wa dini ili Tanzania iwe nchi yenye watu waadilifu na wenye
hofu ya Mungu. Ametoa wito huo Ijumaa, Februari 20, 2015 wakati akizungumza na maelfu
ya waamini na wananchi waliohudhuria ibada ya mazishi ya Askofu Mstaafu Magnus Mwalunyungu
wa Jimbo Katoliki la Tunduru-Masasi kwenye Kanisa la Moyo Mtakatifu wa Yesu. Parokia
ya Tosamaganga, Jimbo Katoliki la Iringa.
“Leo ni siku ya pekee ya kuwasikiliza
viongozi wa dini wakituasa tujiandae kwa maisha baada ya kifo. Tukio hili la leo litupe
nguvu ya kukubali kwamba kifo kipo licha ya kuwa hakizoeleki na kinapotokea kinaleta
simanzi kubwa,” alisema. “Ninawasihi Watanzania wote tufuate mafundisho yanayotolewa
na viongozi wa dini zetu ili Tanzania iwe na kundi la watu wenye hofu ya Mungu, waadilifu
na wanyofu kama ambavyo mahubiri ya leo yamesisisitiza,” alisema.
Waziri
Mkuu ambaye yuko kwenye ziara ya siku tano ya kikazi mkoani Iringa, aliamua kusitisha
ziara yake siku ya leo ili aweze kushiriki msiba huo. Pia alitoa salamu za rambirambi
kwa niaba ya Rais Jakaya Kikwete ambaye yuko Kenya kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi
za Jumuiya ya Afrika Mashariki. Akitoa mahubiri kwenye ibada hiyo, Askofu Damian Dallu
wa Jimbo Kuu Katoliki la Songea alisema wanadamu wanahangaika na kuogopa kifo kwa
sababu hawajui baada ya kifo maisha yao yatakuwaje.
“Askofu Mwalunyungu ameishi
kwa miaka 85 na kati ya hiyo, miaka 55 alikuwa akitumikia kama Padre na kwa miaka
22 alimtumikia Mungu akiwa Askofu. Na hata baada ya kustaafu aliomba awe Parokopale
Kidamalai ambako alitumikia kwa miaka minne. Maisha yake yanaendana na Nenokutoka
kitabu cha hekima kwamba kifo cha mwadilifu ni kupumzika kwa starehe,” alisema.
Ibada
hiyo ya mazishi imehudhuriwa na umati mkubwa wa Maaskofu Katoliki Tanzania pamoja
na waamini kutoka ndani na nje ya Jimbo Katoliki la Iringa.