2015-02-19 09:04:03

Sinodi ya Jimbo kuu la Tabora!


Hivi karibuni, Jimbo kuu la Tabora, Tanzania liliadhimisha Sinodi ya Jimbo iliyokuwa inaongozwa na kauli mbiu " Yesu hu Seba, Taa ya Uhai wa Imani yetu" na hatimaye kuchapicha matunda ya Sinodi ambayo kwa sasa yanafanyiwa kazi na Familia ya Mungu, Jimbo kuu la Tabora. Katika mahojiano maalum na Radio Vatican, Askofu mkuu Paul Ruzoka wa Jimbo kuu la Tabora anazungumzia Ukristo Jimbo kuu la Tabora, amali za Ukristo, Sinodi ya Jimbo, imani, lakini zaidi sifa za Kanisa mahalia. RealAudioMP3

Ukristo Jimbo kuu la Tabora ni matunda ya kazi ya Wamissionari wa Afrika waliofika eneo la Tabora kunako mwaka 1878. Ukristo ni neema, ni ustaajabivu wa Mungu asiyeridhika tu na kuumba ulimwengu na binadamu, lakini anayejishusha katika hali ya kibinadamu, ili kumkomboa mwanadamu kutoka katika lindi la dhambi na mauti.

Jimbo kuu la Tabora katika maadhimisho ya kumbu kumbu ya miaka 60 tangu lilipotambuliwa kuwa ni Kanisa mahalia na Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa Watu, yaani tarehe 25 Machi 1953, utume wa kutangaza, kufundisha na kuwatakatifuza Watu wa Mungu umeendelea kushamiri kwa njia ya Neno la Mungu na Maadhimisho ya Sakramenti za Kanisa.

Askofu mkuu Ruzoka anasema imani inadhihirika katika utendaji na kwamba, imani ya Kikristo inapata chimbuko lake katika haki ya Mungu inayookoa. Anasimulia kwa kina na mapana sifa za Kanisa mahalia: uongozi; hali ya kujitanua na hatimaye kujitegemea.

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.







All the contents on this site are copyrighted ©.