2015-02-13 08:06:47

Mapambano dhidi ya Ebola!


Jumuiya ya Kimataifa inatarajiwa kufanya mkutano mkuu hapo tarehe 3 Machi 2015, huko Brusseles, Ubelgiji ili kupembua kwa kina na mapana hali halisi ya ugonjwa wa Ebola na mapambano yake pamoja na kuibua mbinu mkakati utakaotokomeza kabisa ugonjwa wa Ebola ambao umekuwa ni tishio kwa maisha ya wananchi wengi duniani, lakini kwa namna ya pekee katika Nchi za Afrika Magharibi.

Mkutano huu utaratibiwa na viongozi wakuu wa nchi kutoka Guinea, Sierra Leone, Liberia, Togo, Umoja wa Mataifa pamoja na Jumuiya ya Uchumi ya Nchi za Afrika Magharibi, ECOWAS. Kutakuwepo na wajumbe 80 kutoka Umoja wa Afrika, Umoja wa Ulaya pamoja na Mashirika ya Umoja wa Mataifa ambayo yanajikita katika mapambano dhidi ya janga la Ebola duniani, bila kuisahau Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa. Taarifa zinaonesha kwamba, hadi sasa kuna zaidi ya wagonjwa 22, 000 walioambukizwa Virusi vya Ebola na kati yao wagonjwa 8. 800 wamekwisha fariki dunia.







All the contents on this site are copyrighted ©.