2015-02-03 14:59:33

Kila siku yafaa kusoma na kutafari neno la Injili


Baba Mtakatifu Francisko amesema kutafakari injili kila siku , husaidia kujijenga katika tumaini la kweli. Ni msisitizo aliotoa mapema Jumanne asubuhi wakati akiongoza Ibada Misa katika Kanisa dogo la Mtakifu Marta la hapa Vatican. Papa amehimiza waamini kupata muda wa kusoma Injili kila siku hata kwa hata dakika 10 tu, kupata muda wa kuzungumza na Bwana, badala ya kupoteza muda wote kutazama michezo na maigizo ya wasanii katika vyombo vya mawasilano au kusikiliza porojo za mitaani muda wote

Papa alieleza kwa kutazama ni ipi misingi ya matumaini ya Mkristo. Na alitoa jibu kwamba, ni kuitazama sana sura ya Kristo . Homilia ya Papa ilisonga mbele kwa kutazama kifungu kutoka Waraka Mtume Paulo kwa Waebrania ambacho kinalenga juu ya matumaini. Papa alitafari na kueleza kuwa bila kusikiliza sauti ya Bwana,mtu huwa na uwezekano kidogo sana wa kujenga tumaini kwa yaliyo mazuri zaidi kwa siku za baadaye. Na hivyo akamtaka kila muumini kujifunza jinsi ya kujiweka chini ya ulinzi wa Yesu, kuwa na matumiani kwa Yesu. muhimu kufanya "maombi na kutafakarjuu ya neno la Injili na hili linaweza kufanyika, kwa kuwa na moyo wa kuisoma Injili.

Papa amehoji kwa vipi inaezekana leo hii kuitafakari Injili ? na kutoa jibu kwamba ni kwa kumweka esu akilini mwetu muda wote, Kutambua kuwa Yesu yu pamoja na watu wake muda wote. Yesu muda wote akiwa hapa duniani alikaa kati ya umati wa watu. Na daima alitembea na watu barabara, aliandamana na watu. Na hata katika usafiri wa maji aliandamana na watu, kama injili inavyosema, alikuwa amelala juu ya mashua lakini dhoruba alipokuja na wanafunzi wake wakamwamsha. Na ndivyo inavyotakiwa pia hata siku hizi kutambua kwamba, Yesu yu karibu yetu. Anasubiri tumwamshe na kumwambia, Bwana dhoruba inatuangamiza, naye atauliza pepo zote.

Papa aliendelea kutazama somo la Injili ya leo, akisema , Yesu anatambua kwamba mwanamke mgonjwa katika umati wa watu amemgusa. Tukio hili linatuhimiza kufanya bidii za kuwa karibu na Yesu, kugusa hata upinde wa vazi lake naye atatuponya. Ni kufanya kumbukumbu katika njia yote ya mapito ya maisha, na kumbukumbu ya neema nyingi tulizo pokea kutoka kwa Bwana. Ni kuwa na matumiani na Bwana, ambaye ni mmoja tu, mwenye uwezo wa kutupa matumaini mapya. Nikumtazama sana Bwana , kumjua Bwana, na kuitafakari Injili na kusali kwa ajili ya tafakari hii,. Papa ameomba kila mmoja tangu leo ajaribu kupata muda wa dakika kumi tu, kwa ajili ya kusoma Injili na kufikiria juu yake na kisha kusema , kila jambo namwachia Yesu.








All the contents on this site are copyrighted ©.