2015-02-02 15:48:32

Wiki la jamii: Wadominicani nchini Angola wasisitiza nafasi sawa kwa wote


Taasisi ya Mosaiko Angola, inayoendeshwa na Watawa Wadomenican, Jumamosi tarehe 31 Januari walikamilisha Wiki la Jamii , na msisitizo wa Fursa Sawa, kwa raia wote wa Angola. Wiki la Jamii lilianza Jumanne Januari 27 na kumalizika Jumamosi Januari 31, 2015, katika Mji Mkuu wa Luanda. Malengo ya siku hizi tano, ilikuwa ni kutafakari na kuongeza ufahamu miongoni mwa washiriki, juu ya umuhimu wa majukumu ya kijamii na kutafuta njia halisi za kushuhudia injili ya Kristo katika dunia ya leo.

Taarifa kutokea Washiriki wa tukio hili la wiki nzima, imeeleza kuwa kati ya yalijitokeza,licha ya masuala ya kiroho pia masuala mbalimbali yanayogusa mioyo ya watu katika maisha sambamba na masuala ya kiroho ikiwa ni pamoja na ukosefu wa fursa sawa katika jamii , kuanzia sera za Serikali juu ya kukuza usawa kwa wote na usawa wa kijinsia kwa ujumla; fursa sawa katika matumizi ya rasilimali; demokrasia ya kiuchumi na maendeleo ya binadamu; mapambano dhidi ya umaskini na dosari zingine katika Angola ya Waangola , vilevile wajibu wa Kanisa katika uendelezaji wa fursa sawa kwa wote.

Ingawa Wiki ya kijamii, asili yake ina nia za Kikanisa, lakini limeonekana kuwa kama tukio wazi la kijamii, ambamo sauti za Waangola wote ziliweza kusikika.

Taasisi Mosaiko, hulenga kukuza maelewano na kujenga nguzo za ushirikiano wa baadaye ndani ya Angola. Ilianzishwa mwaka 1997 na wamisionari Dominikani, vikariati ya Angola mara ya kwanza kama taasisi wasi kwa ajili ya kukuza haki za binadamu nchini Angola. Na kazi zake hufanikishwa kwa nguvu ya watu kujitolea, katika kueneza heshima kwa utu wa binadamu na maendeleo ya jamii ya Angola. Ni hasa hulenga katika ufanikishaji wa wananchi wote wa Angola, kushiriki katika mchakato wa kidemokrasia. Hayo yameelezwa na Bruda Julio Candeeiro, OP ni mkurugenzi wa sasa wa Taasisi Mosaiko.








All the contents on this site are copyrighted ©.