2015-02-02 09:29:38

Wajumbe wa Sinodi kutoka Afrika!


Baba Mtakatifu Francisko ameidhinisha orodha ya majina ya wawakilishi wa Mabaraza ya Maaskofu Katoliki kutoka sehemu mbali mbali za dunia, watakaoshiriki katika maadhimisho ya kumi na nne ya Sinodi ya Maaskofu kuhusu Familia, yatakayofanyika mjini Vatican kuanzia tarehe 4 hadi tarehe 25 Oktoba 2015 kwa kuongozwa na kauli mbiu "Wito na utume wa Familia ndani ya Kanisa na Ulimwengu Mamboleo".

Ifuatayo ni orodha ya majina ya Maaskofu kutoka Barani Afrika:
1. Burundi: Askofu Gervais Banshimiyubusa, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Burundi na msaidizi wake ni Askofu Joachim Ntahondereye wa Jimbo Katoliki Muyinga.

2. Ethiopia na Eritrea: Askofu Tsegaye Kenen Derera, Jimbo Katoliki la Soddo na msaidizi wake ni Askofu Markos Gebremedhin, Jimbo Katoliki la Jimma Bonga, Ethiopia.

3. Ghana: Askofu mkuu Gabriel Charles Palmer-Buckle, Jimbo kuu la Accra, na msaidizi wake ni Askofu Anthony Kwami Adanuty, Jimbo Katoliki la Keta Akatsi.

4. Kenya: Kardinali John Njue, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya; Askofu James Maria Wainaina Kungu, Jimbo Katoliki la Muranga. Msaidizi wake ni Askofu Emmanuel Barbara wa Jimbo Katoliki Malindi.

5. Madagascar: Askofu Dèsirè Tsarahazana, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Madagascar. Msaidizi wake Jean de Dieu Raoelison, Askofu msaidizi wa Jimbo kuu la Antananarivo.

6. Rwanda: Askofu Antoine Kambanda, Jimbo Katoliki la Kibungo na msaidizi wake ni Askofu Smaradge Mbonyintenge, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Rwanda.

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.







All the contents on this site are copyrighted ©.