2015-02-02 15:40:16

Kufungwa jela hakuondoi heshima ya utu wa mtu.


Padre Sandro Spriano, Mchungaji wa Kiroho katika gereza Kuu la Rebbibia la Jiji la Roma hivi karibuni katika mahojiano na Allesandro De Carolis wa Redio Vatican, alieleza nia ya Kanisa kuendelea kuwajali hata wahalifu waliofungwa gerezani, akisisitiza kwamba ni muhimu kuwajali wafungwa, kwani kufungwa hakupunguzi thamani ya utu wa mtu.

Na gereza ni mahali na wakati muafaka, ambamo mfungwa anaweza kuona makosa yake na kwa urahisi pia akipata mwongozo mzuri wa maisha, hasa vijana, huweza kujenga maisha mapya ya heshima, kwa wengine.
Mama Kanisa kupitia kazi zake za Kichungaji katika magereza, hutazama kwa kina, mazingira wanamoishi wafungwa , na maisha ya gerezani kwa ujumla, na hitaji la mfungwa mmojammoja, na hivyo kuona kipi kinachotajika zaidi katika kumsaidia kiroho, kwa ajili ya kubadili mwenendo wake wa maisha. Kwa Makasisi wanaotoa huduma magerezani, wanahitaji kuifanya kazi hii kwa tahadhari na mshikamano, ili kumsaidia mfungwa kubadili maisha yake na hivyo kuweza hata kupunguza maisha yake ya kukaa jela.

Na hivyo, lengo kuu la uwepo wa Makasisi magerezani , ni kusaidia wafungwa, wote vijana na watu wazima, kuutazama ukweli wa maisha yao ya nyuma, ili katika ukweli wa yale waliyoyatenda hadi kuwafikisha jela, waweze kuona umuhimu wa kutoa maamuzi thabati katika kuachana na uovu ambao hauwapeleki mbali kimaisha, wabadili mwendo huo na kuchukua mwelekeo mpya wa maisha yaliyo bora zaidi yenye kukubalika kijamii.

Padre Spriano anasema, wao kama makuhani, hutoa huduma yao kwa kadri ya taaluma yao, na hivyo huwavutia wafungwa wengi, kutafakari juu ya maisha yao. Na huduma hii ni muhimu kwa Makasisi wote , kwa kuwa iwapo watawanyanyapaaa wafungwa, basi huduma yao inakuwa sawa na bure. Mfungwa ni mtu mpweke anayehitaji klla kuonyeshwa njia mpya na kiufarijiwa na wengine, Ni muhimu wafungwa kupata huduma ya kuponywa kwa faraja za kiroho.
Makasisi huanza kazi hii yakubadili maisha ya mfungwa, kwanza kupitia uwezekano wa mazungumzo ya ana kwa ana, kw akuzingatia kwamba, idadi kubwa ya vijana na watu wazima hutoka katika kila aina ya maisha , wale waliokuwa. Kuna wakiishi pembezoni mwa jamii, waliokuwa wakinywa haki msingi za maisha, wale waliokuwa wamezongwa na umaskini na upweke, na wengine walikuwa katika hali nzuri lakini wakiishi na moyo wa kutoridhika n.k.. Na hivyo, katika safari hii ya maisha, Makuhani huanza hasa na njia za kusikiliza matatizo ya wafungwa, na baadaye, kutoa majibu kwa matatizo hayo kwa njia tofautitofauti kulingana na haja za wafungwa. Ni jambo la ajabu kwamba wafungwa wengi husikiliza na kuanza kubadili mwelekeo wa maisha yao wakiwa bado gerezani.
Padre Spariano ameeleza huku akiomba sala zaidi kwa ajili ya ndugu hawa walio magerezani, ili roho zao ziweze kulainika na kumfungua mlango ili roho wa Kristo, mwenye uwezo wa kuyabadili maisha yao, iwapo watapenda kwa hiari yao kufanya hivyo, aingie ndani mwao. Na kwamba, Injili haizuii haki za Mahakama kutendeka kwa mkosaji, lakini husaidia mkosaji kutorudia makosa katika maisha yake.








All the contents on this site are copyrighted ©.