Baba Mtakatifu Francisko ametuma ujumbe wa pongezi na shukrani kubwa kwa Shirika la
Misaada la Kanisa Katoliki, Jimbo Katoliki la Mondonedo-Ferrol, lililoko nchini Hispania,
kwa kuadhimisha Jubilee ya miaka 50 tangu lilipoanzishwa. Baba Mtakatifu analipongeza
kwa kuonesha ushuhuda wa upendo na huduma kwa maskini na wote wanaosukumizwa pembezoni
mwa jamii.
Baba Mtakatifu katika ujumbe ulioandikwa kwa niaba yake na Kardinali
Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican, anampongeza Askofu Manuel Sanchez Monge pamoja
na wajumbe wote wa Caritas Jimboni humo na kuwataka kuendelea kushuhudia huduma ya
upendo, inayoonesha neema na upendo wa Mungu kwa waja wake; huduma ambayo ni hai kabisa
ndani ya Kanisa.
Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S. Idhaa ya Kiswahili
ya Radio Vatican.