Pangua pangua ya Rais Jakaya Kikwete Baraza la Mawaziri
Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa Tanzania amefanya mabadiliko katika Baraza la mawaziri
na kuwaapisha Mawaziri wapya. Katika mabadiliko hayo Raisi Kikwete amemteua muheshimiwa
George Simbachawene kuwa Waziri wa nishati na madini, awali alikuwa naibu waziri wa
ardhi.
Wengine walioteuliwa ni Dokta Harisson Mwakyembe ambaye amekuwa waziri
wa ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, mzee Samweli Sita ameteuliwa kuwa waziri wa
Uchukuzi.
Katika mabadiliko hayo pia Rais amemteua mhandisi Christopher Chizza
kuwa Waziri wa nchi uwekezaji na uwezeshaji huku Dokta Maria Nagu akiteuliwa kuwa
Waziri wa nchi mahusiano na uratibu.
Katika mabadiliko hayo pia Mshemiwa Stephen
Wasira ameteuliwa kuwa Waziri wa kilimo, chakula na ushirika huku Williamu Lukuvi
akiteuliwa kuwa Waziri wa ardhi nyumba na makazi. Kwa upande wa Naibu waziri, Anne
Kilango Malecela ameteuliwa kuwa naibu Waziri wa elimu, Ummy Mwalimu ameteuliwa kuwa
Naibu waziri wa Sheria huku Stephen Masele akiteuliwa kuwa Naibu Waziri ofisi ya Makamu
wa Rais Mazingira. Mawaziri hao wanaanza kazi mara moja.