2015-01-22 15:17:30

Papa akutana na ujumbe wa kiekumene kutoka Finland


Baba Mtakatifu Francisko amekutana na ujumbe wa Kiekumene kutoka Finland, kwa kuonyesha furaha yake na kwa moyo mkunjufu aliwakaribisha na kuwatakia kila la heri katika hija yao ya kila mwaka hapa Roma, kwa ajili ya kusherehekea sikukuu ya Mtakatifu Henrik, msimamizi wa Nchi yao. Papa alionyesha kufurahia zaidi kwamba, kwa mwaka huu, hija hii imekuwa kweli tukio kiroho na kiekumeni , kwa uwepo pia mkutano kati ya Wakatoliki na Walutheri, tukio ambalo limekuwa likifanyika kila mwaka sasa karibia miaka 30.

Katika hotuba yake, Papa Francisko, alirejea utendaji huu unaoelekea kutimiza miaka 30, tangu Makatifu Yohana Paulo II, alipokutana kwa mara ya kwanza na ujumbe wa kiekumeni kutoka Finland, uliofika hapa Roma, na aliwapokea kwa maneno haya: "Ukweli ni kwamba, kuja kwenu kwa pamoja hapa Roma, tayari ni ushuhuda umuhimu katika juhudi za kuwa na umoja . Na Ukweli kwamba, wamekuwa pamoja katika kutolea Ibada na sala inakuwa ni ushuhuda katika imani yao kwamba, ni tu kwa neema ya Mungu Wakristo wanaweza kufikia umoja. Na ukweli kwamba, wameweza kuikiri sala ya Imani kwa pamoja ni ushuhuda wa imani moja kwa kanisa zima la Kristo.

Papa Francisco amekumbusha kwa kuitaja hatua hii ya kwanza muhimu ya kiekumeni katika safari kuelekea umoja kamili na ya kuonekana ya Wakristo nchini Finland, lakini pia akasema, bado kuna mengi ya kufanywa kwa ajili ya kukuza umoja huu wakutembea pamoja kama Wakristo kuelekea ushirika kamili katika ukweli na upendo kama alivyoandika Mtakatifu Yohane Paulo II katika waraka wake wa kitume wa Enc Ut unum sint.

Aidha Papa Francisco, ameifurahia ziara yao wanaoifanya sambamba na Wiki la Maombi kwa ajili ya Umoja wa Kikristo, ambalo kwa mwaka huu, linaongozwa na Yesu alizungumza kwa mwanamke msamaria kisimani: "Nipe kinywaji" (Yoh 4,7). Papa Francisco anasema, tukio hili, linatukumbusha kuwa, chanzo cha neema zote ni Bwana mwenyewe, na kwamba ni zawadi yake yenye kuleta mabadiliko katika maisha kwa wale ambao hulipokea Neno na kutoa maamuzi ya kuliisho, wanakuwa mashahuda wa maisha halisi ambayo huja tu kutoka kwa Kristo. Kama Injili inavyo sema, Wasamaria wengi walimwamini Yesu kwa ushuhudi wa mwanamke Msamaria
.
Papa Francisco pia alitaja kama alivyobaini Askofu Vikström, Wakatoliki na Walutheri unaweza kufanya mengi kwa pamoja, katika kuishuhudia huruma ya Mungu katika jamii yetu. ushuhuda wa pamoja wa Kikristo, unahitaji kuonekana hasa katika uso wa kutoaminiana, uso wa ukosefu wa usalama, mateso na madhulumu, na utendaji mbovu wa watu wengi katika dunia ya leo.

Papa ameendelea kuzungumzia ushuhuda huu pamoja kwamba, , unaweza kuungwa mkono na kuhimizwa na kusonga mbele kwa majadiliano ya kiteolojia kati ya Makanisa. Na Azimio la Pamoja juu ya mafundisho ya kuhesabiwa haki, lililotiwa saini rasmi zaidi ya miaka kumi na tano iliyopita kati ya Shirikisho la Dunia la Waluteri,na Kanisa Katoliki la Roma, vinaweza kuzaa matunda zaidi ya maridhiano na ushirikiano.








All the contents on this site are copyrighted ©.