2015-01-22 07:49:09

DRC kunawaka moto!


Kardinali Laurenti Monsengwo Pasinya, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Kinshasa, DRC amekemea sana mauaji ya watu wasiokuwa na hatia yaliyofanywa na vikosi vya ulinzi na usalama katika harakati za kusimamisha mchakato wa mabadiliko ya Katiba unaotaka kutoa mwanya kwa Rais Joseph Kabila, ambaye amekuwepo madarakani kuanzia mwaka 2001 kuendelea kukaa madarakani. Kardinali Monsengwo anasema, si haki kwa vikosi vya ulinzi na usalama kuua raia ambao, wanapaswa kuwalinda na kuwatetea.

DRC kunawaka moto kwa wananchi kuonesha nguvu ya umma ili kupinga mchakato wa kutaka kupindisha Katiba, ili kutoa mwanya kwa Rais Joseph Kabila kuendelea kuwa madarakani. Wananchi katika patashika nguo kuchanika, wanaendelea kukumbana na rungu la dola.

Baraza la Maaskofu Katoliki DRC linapinga mchakato wa kutaka kupindisha Katiba ya nchi kwa ajili ya mafao ya watu wachache ndani ya jamii na kwamba, wananchi nao wanapaswa kutumia njia za kidemokrasia na amani, ili kuhakikisha kwamba, utawala wa sheria unalindwa na kuzingatia, vinginevyo, DRC itaendelea kuwa ni uwanja wa fujo, mwenye nguvu mpishe! Jumuiya ya Kimataifa inaitaka Serikali ya DRC kuheshimu Katiba.







All the contents on this site are copyrighted ©.