Mpendwa msikilizaji wa kipindi chetu cha Kanisa la nyumbani, Tumsifu Yesu Kristo.
Kwa mara nyingine tena tunakukaribisha uendelee kukitegea sikio kipindi chetu pendevu,
ili tuisikie sauti ya Mama Kanisa anayetuelekeza nini cha kufanya ili Kanisa lizidi
kuwa hai na Injili ya Kristo isonge mbele kwa ajili ya wokovu wa ulimwengu. 00:09:55:27
Baada ya
kuongelea Maaskofu, Mapadre na Watawa katika vipindi vilivyopita, leo tunawatupia
jicho waamini walei kwa kuutazama utume wao ndani ya Kanisa na kwa ulimwengu, kama
tusomavyo katika hati ile iitwayo kwa lugha ya Kilatini ‘Apostolicam Actuositatem’
yenye kumaanisha Utendaji wa Kitume.
Tutakumbuka kwamba, Mtaguso Mkuu wa II
wa Vatican ndiyo uliotoa sura mpya ya Kanisa, yenye kulionesha kanisa kama Watu wa
Mungu, Familia ya Mungu au Mwili wa fumbo wa Kristo. Hayo yote yalikuwa ni kujaribu
kuonesha Kanisa kama Muungano kamili wa Wabatizwa wote, ambapo tunaishi na tunasafiri
pamoja katika hija yetu ya hapa duniani. na lengo la u-pamoja wetu ni kusaidiana,
kuimarishana, kutegemezana, kutakatifuzana, kuyatakatifuza malimwengu na sisi wenyewe
kuendelea kufanywa watakatifu. Wajibu huu ni wa waamini wote na una msingi katika
Ubatizo wetu.
Ndiyo maana katika Hati hii, Mtaguso wa pili wa Vaticani uliwaongelea
walei kwa namna ya pekee na ukionyesha nafasi yao katika maisha ya . Hati hii ni
mwongozo wa Utume wa Walei katika Kanisa na Ulimwengu. Mtaguso unasema, sisi waamini
walei, tuna nafasi kubwa sana ya kushiriki katika utume wa Kanisa katika nyanja mbalimbali,
kama vile katika familia zetu, katika Jumuiya za Kanisa, katika mazingira mbalimbali
ya kijamii na pia katika maeneo yetu ya kazi, ambako twaweza kupeleka cheche za Injili
ya Kristo kwa maneno na matendo na zaidi sana kwa mfano wa ushuhuda wa maisha yetu
ya kila siku, yenye kutoa mirindimo ya Injili ya Kristo.
Katika nyanja hizo,
sisi walei tunatumwa kutekeleza utume wa kuinjilisha na wa kutakatifuza, kukoleza
zaidi roho ya Kikristo katika ulimwengu na kuzidisha zaidii matendo ya huruma. Ni
kwa njia hiyo nasi walei tutakuwa tunamfuasa Kristo anayesali, anayefundisha, anayewahurumia
na kuwasaidia wenye shida na anayeeshiriki maisha yake na ulimwengu.
Mtaguso
mkuu wa Pili wa Vatican, ulitazama kwa kina na kuona kwamba, asilimia kubwa ya waamini
wote wa ni walei, tena ndio wanaoshirikiana zaidi na watu wowote katika mambo mengi.
Hivyo wasipotoa mchango wao, utume wa Kanisa utadumaa. Mwamimi mlei kwa hulka yake
na uwezo wake na kwa fursa ya mazingira ya maisha yake, ana nafasi kubwa sana ya kuuinjilisha
Ulimwengu. Akitekeleza wajibu huo kwa moyo na kwa kushirikiana na miongozo mbalimbali
ya Kanisa, hapo kazi ya Uinjilishaji itasonga mbele.
Mtaguso mkuu wa Pili wa
Vatican unatuelekeza, ili kweli sisi walei tuweze kutimiza utume wetu vizuri, tujibidishe
kwanza kabisa kuurutubisa Ukristo wetu uliojengeka katika ubatizo kwa kukoleza maisha
yetu ya kiroho, maisha yetu ya muungano binafsi na Mungu. Huu ni mwito wa kila siku
kujaribu kuuambata uongofu wa kweli. Ni kwa njia hiyo, tutaweza kutekeleza utume wa
kuwasaidia wengine pia.
Mtaguso unasisitiza kwamba, utume wetu sisi walei,
sio tu kueneza ujumbe wa , bali pia kuratibu malimwengu yafuate , kutimiza matendo
ya na kushuhudia . Nyakati zetu hizi zinashuhudia hali ya aibu katika kushuhudia
Injili ya Kristo, na wakati mwingine watu kushindwa kuwianisha tunu za Injili wanazozisadiki
na maisha halisi ya utendaji ya kila siku. Kiujumla ni kushindwa kuyamwilisha mafundisho
ya Kristo katika maisha yetu ya kila siku.
Na kibaya zaidi, kunazidi kukua
roho ya ubinafsi-angamivu, ambapo tunashuhudia vitendo vya biashara haramu ya binadamu,
utumwa mamboleo, biashara za bidhaa za vitu hatarishi na angamizi kwa usitawi wa binadamu,
upandikizwaji wa vita na magonjwa kati ya watu, upandikizwaji wa itikadi na mifumo
angamizi kwa mustakabali wa familia ya mwanadamu; haya na mengineyo mengi kama hayo,
ni dalili za kukosekana kwa utume makini wenye kuzaa matunda kati ya watu.
Tunasema
hivyo kwa sababu wanayotenda hayo, baadhi yao ni sisi tunaomsadiki Kristo. Kwa mwangwi
wa hati hii, mwito kwetu sote kupenyeza roho ya Kikristo katika maisha yetu ya kila
siku na katika mazingira yote ya watu.
Mtaguso unatueleza pia namna za kutimiza
utume huo, kuanzia ule kwa mtu mmojammoja hadi ule wa pamoja katika vyama mbalimbali
ambavyo walei wana haki ya kujiundia, na katika miundo maalumu iliyoanzishwa na wachungaji
wao au wanayojianzishia wenyewe kwa kufuata taratibu za Kanisa. Kila mtu kwa nafasi
yake anaalikwa kufanya utume kwa kutangaza injili na kutakatifuza, iwe ni kwa mtu
mmoja au kwa kundi la watu. Na pia inahimizwa sana kutekeleza utume huo katika umoja,
kwa njia ya vyama vya kitume. Vyama vya kitume ni msaada mkubwa sana katika kujiendeleza
sisi wenyewe kiroho na pia katika kuunganisha nguvu zetu za uinjilishaji wa kina kwa
pamoja.
Mtaguso unatuelekeza pia utume huo tuutende kwa utaratibu wenye kuongozwa
na roho wa Mungu, na sio katika roho ya na mashindano bali kwa upendo na , kwanza
na maaskofu, mapadre na wahudumu wengine mpaka na wa tofauti na wasio Wakristo.
Mpendwa msikilizaji, mara nyingi wivu na mashindano yenye majivuno, vimekuwa
ni baadhi ya mambo yanayokwamisha kabisa kazi ya Injili. Mahali penye wivu, kazi ya
Mungu hukwama kwa sababu, watu tunatumia muda mwingi kuoneana wivu, kusemanasemana,
kuharibiana kazi, kutafutatafuta makosa, badala ya kufanya mambo ya msingi. Mashindano
yenye harufu ya ubinafsi, kujitutumua, kutafuta umaarufu na sifa, na kudharau wengine,
kunyanyapaa wanyonge na maskini, navyo vimekuwa ni kikwazo kikubwa sana katika utume
wa walei. Lengo la utume wetu sisi walei ni kushiriki katika kazi ya ukombozi wa
mwanadamu kimwili na kiroho.
Sisi walei tutekeleze utume wetu ndani ya Kanisa
kwa namna ya kufikiri pamoja na Kanisa na kutenda kadiri ya Miongozo ya Kanisa. Tukiwa
tayari kutoa ushirikiano mnyoofu kwa viongozi wetu wa Kiroho, na sisi wenyewe tukijibidisha
kutekeleza yale tunayopaswa kutenda, hapo utume wetu utakuwa hai zaidi na zaidi. Daima
tufungue macho, ili kwa mwanga wa Injili tuone ni maeneo yapi haswa tunapaswa kupenyeza
Injili ya Kristo zaidi na zaidi.
Hati hii inahitimishwa kwa kusisitiza sana
malezi bora ya utotoni na ujanani. Roho ya utume ndani ya Kanisa hufundishwa na kupandikizwa
tangu utotoni. Hivyo watoto wasiachwe nyuma na Vijana nao waangaliwe kwa umakini.
Malezi ya kiutu na Kikristo yapatiwe mkazo zaidi. Hayo husaidia sana kumuunda mtu
anayefaa na anayejali utu. Malezi ya kitaaluma peke yake, pasipo utu wala dhamiri
hai kwa Mungu, ni hatari kwa watoto wetu.
Ninakualika mpendwa mwamini mlei,
kufufua na kukuza sana ile roho ya uwajibikaji ndani ya Kanisa na katika mazingira
yote yalioainishwa. Mahali popote tuwapo, tuwe wakristo hai, na kwa roho ya umoja
na uwajibikaji wa kweli, tutimize wajibu wetu vema.
Kutoka katika Studio za
Radio Vatican, ni mimi Padre Pambo Martin Mkorwe, OSB.