2015-01-12 07:51:31

Je, wewe?


Mpendwa Msikilizaji wa Kipindi chetu cha Kanisa la nyumbani, Tumsifu Yesu Kristo! Karibu kwa mara nyingine tena tuendelee kufikiri na Kanisa kwa njia ya ujumbe wa hati za Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vaticani. 00:10:33:41 RealAudioMP3

Leo tunaitazama hati ile inayohusu upyaishwaji wa maisha ya Kitawa inayojulikana kwa jina la Kilatini Perfectae Caritate, ikimaanisha Mapendo Kamili. Hati hii inatoa maelekezo ya jumla kwa watawa na maisha ya kitawa ndani ya Kanisa, kwa lengo la kuwafanya watawa na utume wao viendani na fikra za Kanisa na mahitaji ya mazingira.

Tufahamu kwamba, utawa ni mfumo wa maisha ndani ya Kanisa ambamo, baadhi ya wabatizwa waume kwa wake, huitwa na Mungu na kuishi maisha ya kitawa kwa kufuata mashauri ya Injili, huku wakiongozwa na Upendo kwa Mungu na jirani, dhana inayojionesha katika maisha na huduma yao kwa Kanisa na Ulimwengu. Ni kwa namna hiyo, tunaona kwamba kiini haswa cha maisha na utume wa Mtawa ni kujishikamanisha na Mungu ili kuweza kuyatakatifuza malimwengu. Watawa wanayatakatifuza malimwengu kwa njia ya Mfano wa maisha yao ya kujisadaka, kwa njia ya sala zao na huduma zao, huku wakiufuasa mfano wa Kristo mwenyewe aliyekuja si kutumikiwa bali kutumikia.

Kwa mujibu wa taratibu zetu, mbatizwa yeyote, mwenye kujisikia wito wa utawa huweza kujiunga na shirika lolote la Kitawa. Kuna aina mbalimbali za mashirika ya kitawa ndani ya Kanisa. Kuna mashirika yanayoshughulika na kusali tu katika na u; kuna mashirika yaliyoanzishwa ili kutimiza huduma maalumu kwa niaba ya na kama sehemu ya maisha yao ya kitawa; pia kuna mashirika yanayotakiwa kuunganisha kiaminifu ratiba ya sala na taratibu nyingine za kijumuia pamoja na fulani.

Kuna mashirika ya kikleri na mashirika ya kilei. Yapo mashirika ya watawa wa kiume tu (pasipokuwa na mapadre ndanimwe), kuna mashirika ya kitawa ya kike na kuna yanayotafuta kwa kuishi katika mazingira ya kawaida ya watu, pasipo kujitenga na kwenda kuunda jumuiya.

Mashirika hayo yote yanaongozwa na Karama maalum ya mwanzilishi na watawa huiishi Karama hiyo kama inavyotambuliwa na Kanisa. Na watawa hao hujishikamanisha na maisha hayo kwa vifungo vya nadhiri zenye msingi katika mashauri ya Injili au vifungo vingine vitakatifu, lengo likiwa ni kumtafuta Mungu kwa njia ya kumfuasa Kristo kwa ukaribu zaidi kwa njia ya kuyaishi mashauri hayo ya Injili.

Hao wote wanamfuasa Kristo yule yule. Wapo wanaomfuasa Kristo anayesali, wapo wanaomfuasa Kristo anayefundisha, wapo wanayemfuasa Kristo anayeponywa wagonjwa, wapo wanayemfuasa Kristo anayehubiri Habari Njema ya Ufalme wa Mungu, wapo wanaomfuasa Kristo anayewatendea mema watu, na wapo wanaomfuasa Kristo anayeshiriki maisha ya watu. Ni kwa mtazamo huu ndio tunakuta kuwa tuna mashirika mengi yenye karama tofauti-tofauti ndani ya Kanisa. Watawa wote kwa njia ya huduma zao, wanachangia katika maisha, usitawi na utakatifu wa Kanisa.

Ni kwa sababu ya uzito huo wa maisha ya Kitawa, Mtaguso Mkuu uliona ni vema ukayapatia maisha ya kitawa mwongozo kamili, ili maisha hayo ya kitawa yapate maana chanya zaidi ndani ya Kanisa. Mtaguso ulisisitiza hali mpya ya inayopaswa kuonekana katika mambo makuu matano yaani: kushika kama kuu, kufuata kiaminifu ya na bora ya , kujihusisha na maisha na malengo yote ya Kanisa, kupima hali na mazingira ya watu wa leo, kuweka mbele kuliko mambo mengine. Ni kwa mtazamo huo tu, ndio watawa wataweza kumwilika katika Kanisa na mazingira na nyakati halisi.

Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican uliwahimiza watawa kushika , kujikatalia malimwengu, kujiwekwa kwa juu ya msingi wa , kulitumikia Kanisa, kutekeleza , kumfuata kwa bidii kama jambo pekee na la lazima, na kuunganisha maisha ya na moyo wa kitume. Kupenda kufanya kazi ndani ya Kanisa na kwa ajili ya Kanisa, kwani mashirika yote ya Kitawa ndani ya Kanisa ni mali ya Kanisa, ni mikono ya Kanisa. Hivyo utume wowote ulenge katika kushiriki kazi ya Kanisa ya kumkomboa mwanadamu kiroho na kimwili.

Mpendwa msilikizaji wa Kipindi chetu cha Kanisa la Nyumbani, tunakuletea habari hii sasa ambapo Kanisa linaadhimisha Mwaka wa Watawa. Pamoja na mambo mengi ambayo tumefunzwa kuhusu watawa, na sisi kwa upande wetu tuone mambo mawili tu. Kwanza tujibidishe kuyaenzi maisha ya kitawa. Katika uhalisia wake, wengi wetu tumeona na tunathamini na tunahitaji kabisa huduma za watawa. Lakini neno ni lilelile. Watawa ni watoto wetu, wanaitwa kutoka katika familia zetu kwa ajili ya kutuhudumia sisi wenyewe.

Basi, tujibidishe sote katika kulea vizuri watoto wetu ili katika akili tulivu na dhamiri hai, waweze kuisikia sauti ya Mungu anayewaita. Hati hii inasema kuwa jukumu la kulea miito ni la wazazi, watawa wenyewe kwa njia ya mfano wa maisha yao, pamoja na wachungaji wetu wa Kiroho. Sisi wanafamilia, tulizawadie Kanisa letu watawa, ili kazi ya Injili isonge mbele zaidi.

Wakati fulani huwa kunakuwa na wazazi wa ajabu sana, ambao wanapenda sana watawa, na wanapenda watoto wao walelewe na wasome shule za watawa! Na wanastaajabia huduma zinazofanywa na watawa ndani ya Kanisa. Lakini wakisikia kuwa mtoto wao ana wito wa utawa, wanafanya kila aina ya fatiki ili kumkatisha tamaa kupindisha mawazo hayo kwa mtoto huyo. Wapo wazazi na walezi waliomdhulumu Mungu anayeita watu na kulikosesha kanisa Watenda kazi, kwa kuwakataza kabisa watoto wao wasijiunge na maisha ya kitawa.

Pili, kwa mwaka huu tunapoadhimisha Mwaka wa Watawa, waamini wote katika ngazi zote, tuone namna ya kuwashukuru watawa kwa majitoleo yao kwa Kanisa. Namna ya kwanza ya kuwashukuru ni kuwaombea wadumu katika wito wao. Na ya pili ni kuwapa ushirikiano katika utume wao, ya tatu ni kuwalinda wasipatwe na mabaya. Nyakati fulani na katika mazingira fulani watawa wetu wanateswa kweli. Hata kama wapo kwa ajili yetu, wanatuhudumia afya zetu, utashangaa sisi wenyewe ndio tunawapiga, tunawaibia vifaa vya kazi, tunawadhulumu haki zao na mambo kama hayo.

Hapa swala la msingi ni hili: endapo watawa wapo katika maeneo yetu wanatutumikia, sisi watu wa maeneo hayo tuwalinde ili wakae kwa usalama. Na wanapotutumikia, tuwape malipo ya haki, bila kusahau kuchangia matunzo yao uzeeni, ili wasizeeke kwa huzuni baada ya kazi ngumu ya kuwahudumia watu. Tuwajengee watawa wetu mazingira ya amani, ili waishi na kumtumikia Bwana kwa furaha na kwa njia ya huduma zao Mungu Atukuzwe, Ulimwengu Utakaswe na sisi tuokolewe.

Kutoka katika Studio za Radio Vatican, ni Mimi Padre Pambo Martin Mkorwe, OSB.








All the contents on this site are copyrighted ©.