2015-01-08 11:10:32

Hakuna kinachoweza kuhalalisha kitendo cha kuondoa maisha ya mtu


Baada ya kusikia habari ya mashambulizi ya kutisha yaliyofanyika Paris katika makao makuu ya Gazeti la kila wiki la 'Charlie Hebdo' lililosababisha watu kadha kupoteza maisha na majeruhi wengi, Papa Francisko, amejiunga katika maombi, kuombea kafara wa tukio hili na familia nyingi zilizoumizwa na msiba huu.

Katibu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin, kwa niaba ya Papa , amepeleka salaam za rambirambi za Papa kwa wahanga wa tukio hili, ambamo amewakabidhi waathiriwa katika huruma ya Mungu, na kuomba awapokea katika mwanga wake.Na pia anaombea familia zao na majeruhi, wajaliwe faraja za Bwana wakati huu wa mtihani mkubwa.

Baba Mtakatifu analaani, kwa mara nyingine tena, vurugu zenye kusababisha mateso mengi na kumwomba Mungu zawadi ya amani, na kuzitakia familia zilizoathirika zaidi, baraka ya Mungu.

Pia Msemaji wa Vatican, Padre Federico Lombardi, ameviambia vyombo vya habari kwamba, Baba Mtakatifu, analaani vikali shambulio hili la kuchukiza, uhalifu uliotikisa si tu watu wenye mapenzi mema Ufaransa, lakini duniani kote.

Na kwamba, Papa Francisco anatolea zake sala na kushiriki mateso ya kafara, majeruhi na familia kutokana na uhalifu huu , hasa mateso ya familia za mateso ya waliojeruhiwa na familia ya watu waliokufa, na juu ya yote, ametoa wito wa kupinga kwa njia zote, uenezaji wa chuki na aina zote za unyanyasaji, kimwili na kimaadili, ambavyo huharibu maisha ya binadamu, utendaji wowote wenye kukiuka hadhi ya watu, na wenye kuathiri kwa kiasi kikubwa, msingi ya amani na mshikamano mzuri kati ya watu, licha ya tofauti za utaifa, dini na utamaduni.

Hakuna kinachoweza kuhalalisha vurugu zenye mauaji. Mauaji ni adui wa mawazo, na kamwe hayawezi kuhalalishwa kwa kuwa maisha ni heshima ya kila mtu na yanapaswa kulindwa kwa uhakika dhidi ya maamuzi yoyote yaliyo kinyume , yoyote yanayo weza kuleta chuki. Ni lazima kukataa mauaji. Ni lazima kuheshimu maisha na kuyalinda. Papaa ameonyesha ukaribu wake na mshikamano wake wa kiroho na msaada kwa wale wote ambao, kwa mujibu wa majukumu yao mbalimbali, wanaendelea kufanya kazi, kwa ajili ya amani, haki na sheria, uponyaji wa kina wa vyanzo na saba bu zinazoweza kujenga chuki, kama ilivyoonekana sasa Ufaransa na duniani kote kwenye dalili za mvutano na vurugu.
Pia Maaskofu Katoliki wa Ufaransa wametoa tamko lao kufuatia shambulio hili katika jengo la gazeti la Charlie Hebdo, wakisema, “ kitendo hiki ni cha kufedhehesha na si haki”. Maaskofu wa Ufaransa wamelaani kwa nguvu unyama huu na kutoa wito kwa serikali kuwapata wahusika wote na kuwafikisha mbele ya sheria.
Katibu na msemaji wa Maaskofu, Ribadeau Olivier Dumas, ameonyesha hofu ya Maaskofu kwa kile kilichotokea na kwamba wote watakuwa karibu jamaa wa waathirika na wafanyakazi wa gazeti hilo.
Na kwamba hakuna kinachoweza kuhalalisha vurugu hizo, ambazo huathiri uhuru wa kujieleza, msingi muhimu wa jamii ya Ufaransa. Na pia wamewataka wananchi wasitende kwa ghadhabu za kulipiza kisasi , lakini wauishi msiba huu kwa kujenga udugu na mshikamano , kama vipengere muhimu katika udumishaji wa amani .








All the contents on this site are copyrighted ©.