Papa anawashukuru akina Mama wote kwa wajibu wao muhimu kijamii na kiroho!
Baba Mtakatifu Francisko ametoa shukrani zake za dhati kwa wanawake wote, kwa wajibu
na majukumu yao muhimu kijamii, kikanisa na kidunia kwa ujumla. Papa alitoa shukurani
hizo wakati wa Katekesi yake kwa Mahujaji na wageni Jumatano hii, Katekesi iliyofuatia
maadhimisho ya Sikukuu za Kiliturujia za Kanisa, katika kipindi hiki, zikiangalisha
zaidi kwa Mama Bikira Maria , Mama wa Yesu.
Papa ameendelea kuzungumzia familia,
kwa uvuvio wa uwepo wa Mama Maria, Mama yetu anayemwasilisha mtoto wake duniani.
Katika tafakari hii juu ya majukumu ya Mama kwa jamii, na Kanisa Papa anasema, Kanisa
pia ni sawa na Mama , na hivyo ndani yake hakuna muumini yatima. Na wakati huohuo
ametoa wito kwa jamii, kuelewa matatizo na mahangaiko ya Mama katika maisha yake
ya kila siku, ambayo hupambana nayo, katika majitoleo yake ya sadaka ya maisha ,
kwa ajili ya watoto wake.
Papa amekumbusha, ndani ya familia kuna mama ,
na kila binadamu, amepata maisha yake kutoka kwa mama na daima ni mama ambaye hutoa
msaada mkubwa wa malezi katika yote mawili kibinadamu na kiroho pia. Mama, hata
hivyo, kwa mara nyingi, licha ya kuwa na jukumu hili kubwa , katika maisha ya kila
siku, uwepo wake haupewi uzito kama inavyotazamiwa. Na badala yake, mara nyingi majitoleo
yake ya sadaka kwa watoto wao, huchukuliwa kama jambo la kawaida kwa maisha ya kijamii
au hata kupuuzwa.
Papa aliendelea kuonyesha masikitiko yake kwamba, hata katika
jamii za Kikristo, mama si mara zote hupewa haki na heshima anayostahili au kusikilizwa.
Papa ameonyesha kujali na kuiomba jamii, ibadilike, ifanye mageuzi yenye hatua
za kusikiliza na kuelewa malalamiko ya mama , iwe maisha ya kijamii au ndani ya
maisha ya kanisa, mama waungwe mkono.
Lakini pia Papa alionyesha kutambua
uwepo wa mama wachache ambao huvuka hata mipaka yao kama mama na kutenda kama wanaume.
Amesema mama hao, wanakwenda nje ya barabara, na si sahihi kwao, kwa kuwa hujiongezea
mzigo wa majukumu, katika kweli za maisha yao, kama wanawake, na maisha ya kifamilia.
Papa anataja ni umama ni fimbo ya nguvu yenye kusitisha moyo wa ubinafsi
na uchoyo. Papa alifafanua maana ya ubinafsi katika maana ya kutokuwa na moyo wa
kugawana na wengine . Mama mwema daima huwa tayari kugawana na wengine alivyo navyo
kama inavyojionyesha katika shule yake ya malezi kwa watoto wao. Umama Papa anasema
ni zaidi ya kuzaa watoto.Ni uchaguzi wa maisha yenye kuwa na mwelekeo wa kujitolea
sadaka kwa ajili ya wengine, kuheshimu maisha na uwajibikaji katika kurithisha yaliyo
mema na tunu msingi za kidini ambayo ni mambo muhimu kwa jamii adilifu na tulivu.
Papa
ameeleza na kurejea maneno ya Marehemu Askofu Mkuu Oscar Arnulfo Romero aliyesema,
kukubali kuwa mama mzazi ni sawa na kukubali kifo dini.. kama pia ilivyoandikwa katika
mtaguso Mkuu wa pili wa Vatican kwamba, "Sisi wote ni lazima kuwa tayari kufa kwa
ajili ya imani yetu. Papa amezungumzia kwa kina heshima hii ya kuyatoa maisha kwa
ajili ya mwingine akisema ni wajibu na haki katika maisha ya ukimya wa imani, sala
na uaminifu, katika maisha ya kila siku, kuyatoa maisha hatua kwa hatua, kama anavyoyatoa
mama kwa mwanae, bila hofu, wala kuchoka lakini kwa unyenyekevu hata wakati anapojua
kufanya hivyo anaweka maisha yake katika hatari za kifo, huendelea kuwa kuwa shahidi
wa maisha kuzaliwa na kuyahudumia kwa upendo .
Papa anasema Jamii bila mama,
ni jamii isiyokuwa na ubinadamu, kwa sababu mama ni ushuhuda wa kugawana na kushirikishana
yaliyo mema , na hata wakati mgumu, hubaki kuwa chimbuko la huruma, sadaka na nguvu
ya maadili. Mama mara nyingi, ni nguzo katika utendaji wa kidini, ibada na sala,
ambamo mtoto hujifunza, na kuiandika thamani ya imani katika maisha yake. Mama ni
Mpanzi wa wa kwanza wa mbegu ya imani.
Bila mama, Kanisa haliwezi kuwa na
waumini wapya, na imani huwa na mwelekeo wa kupoteza sehemu kubwa ya joto lake kirahisi.
Papa alieleza na kutoa shukurani zake nyingi za dhati kwa mama wote, kwa familia na
pia kwa Kanisa na Dunia.