2015-01-07 11:44:42

Ebola imetikisha maisha na imani ya watu!


Wachunguzi wa masuala ya afya ya binadamu wanasema kwamba, madhara ya ugonjwa wa Ebola Afrika Magharibi yataendelea kudumu kwa muda mrefu na kwamba, watu wanaendelea kupoteza maisha yao kutokana na kuambukizwa kwa virusi vya Ebola. Hadi kufikia mwishoni mwa Mwezi Desemba 2014, zaidi ya watu 8880 walikuwa wameambukizwa virusi vya ugonjwa wa Ebola nchini Sierra Leone.

Taarifa iliyotolewa na Shirika la Habari za Kimissionari, FIDES inaonesha kwamba ni zaidi ya wagonjwa 2529. Licha ya watu wengi kuendelea kupoteza maisha yao, lakini kutokana na juhudi, zaidi ya wagonjwa 1326, wametibiwa na kupona kabisa, tayari wamekwisharudi kwenye familia zao. Madhara ya virusi vya Ebola, vimesababisha madhara hata katika ibada.

Waamini wanapokwenda Kanisani wanapaswa kuosha mikono yao kwa maji yenye dawa, hawaruhusiwi kushikana mikono, wala Sakramenti ya Ubatizo, Mpako wa wagonjwa na Ndoa Takatifu hazitolewi tena. Protokali iliyowekwa inazuia pia mikusanyiko mikubwa ya watu, kwa hofu ya kuambukizwa virusi vya Ebola. Kuna kundi la watoto yatima na watu waliosalimika kupoteza maisha, lakini bado wanabaguliwa na kutengwa na jamii. Ubaguzi pia wanafanyiwa wale wanaohusika na huduma ya mazishi wa ugonjwa wa Ebola! Kwa maneno machache, ugonjwa wa Ebola umetikisha maisha na imani ya watu!







All the contents on this site are copyrighted ©.