2015-01-05 07:44:57

Mwanga wa Mataifa!


Baba Mtakatifu Francisko katika Siku kuu ya Tokeo la Bwana, au Epifania ya Bwana, inayoadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe 6 Januari, anatarajiwa kuadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, kuanzia saa 4:00 za asubuhi kwa saa za Ulaya. RealAudioMP3

Hii ni Siku kuu ambayo Yesu, Mwana wa Mungu alipenda kujifunua kwa mataifa, akawa ni kivutio kikubwa cha wataalam wa nyota kutoka Mashariki wanaojulikana kama Mamajusi kutoka Mashariki ya Mbali. Wataalam hawa wa nyota kadiri ya Mapokeo ya Kanisa wanaitwa: Gaspar, maana yake, mtu mwenye heshima au mwalimu; Melchior jina linalomaanisha: Mfalme wangu ni mwanga na Balthazar maana yake Mungu ayalinde maisha yako! Hii ni Siku kuu yenye utajiri mkubwa katika maisha na utume wa Kanisa, changamoto kwa waamini kuwa kweli ni chumvi ya dunia na mwanga wa mataifa.

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.








All the contents on this site are copyrighted ©.