2015-01-05 12:50:25

Atendaye maovu achukia amani!


Baba Mtakatifu Francisko anahimiza, wakati huu wa mapambazuko ya mwaka mpya, ni wakati wa kuwasha ndani ya mioyo, matumaini mapya ya imani, kwa ajili ya kuwa wajenzi wa amani, mahali popote, siku hadi siku. Papa alitoa himizo hilo wakati wa sala ya Malaika wa Bwana, siku ya Jumapili, ambamo alirudia kusema kwamba, daima kuna uwezekano wa kuelewana, ingawa inaweza kuwa kazi ngumu kwa wale waliobobea katika utendaji wa giza nene la kutengeneza vita.

Papa alieleza akionyesha imani yake kali kwamba, daima kuna mwanya wa maridhiano, hata kama maneno ya mwanga na amani, wakati mwingi humwezwa na hali halisi za wale wanaopendelea giza la maovu na vita. Papa Francisco alirudia kusema maneno hayo, akiendeleleza mafundisho yake, juu ya mwanga na amani, kama alivyoeleza pia katika ujumbe wake wa tarehe Mosi Januari, ambayo ni Siku ya kuombea amani duniani. Maelezo ya Papa, yalizielekea taarifa za ghasia na machafuko zinazotolewa kwa wingi kila siku katika vyombo vya habari vya Kimataifa na kitaifa pia kama vile, amani haiwezi kupatikana bila kuwa na ghasia na vita au bila ya kunyamazisha bunduki. Papa anasema, inawezekana kabisa kuepuka hali hiyo na kuwa na mwanzo mpya wa kutembea katika njia ya mafanikio ya amani kupitia utendaji mbalimbali .

Papa alieleza akiifikiria migogoro mbalimbali yenye kusababisha umwagaji damu katika mikoa mingi duniani , msuguano katika familia na jamii, na hata katika baadhi ya Parokia, mna vita! Na pia alipeleka mawazo yake katika miji mingi ya dunia na nchi kati ya makundi ya vyama mbalimbali ya kitamaduni kikabila na kidini. Papa alitahadharisha kwamba, tunahitaji kujua, licha ya upinzani wote kwamba, maelewano, mara zote huwezekana, katika kila ngazi na katika kila hali. Na kwamba hakuna ustawi bora kwa siku za baadaye bila kuwa na amani .

Papa alieleza na kurejea kiini cha Ujumbe wa Injili ya siku kutoka Injili ya Yohana, pia akiangalisha katika mazingira ya hali ya hewa ya siku ya Jumapili ilivyokuwa katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, ambako maelfu kwa maelfu ya watu walikuwa wamefurika kumsikiliza , na hivyo aliendelea kuzungumzia tofauti ya mwanga na giza, na kukemea unafiki mkubwa wenye kuangamiza watu wengi duniani , kutokana na kukosekana kwa amani duniani.

Alisema, watu huzungumzia juu ya mwanga, lakini wakati huohuo wakipendelea utulivu kudanganyifu wa giza. Mara kwa mara huzungumzia amani lakini wakati huohuo wakichagua vita au kufanya kosa la kukaa kimya, bila jitihada zozote halisi za kujenga amani (...) Kwa kweli , Papa alisisitiza, “Mtu yeyote atendae maovu anauchukia mwanga! Na hatoki katika mwanga kwa kuwa matendo yake si ya mwanga. Atendaye maovu anauchukia amani. "

Papa alieleza kwa kuangalisha pia katika ujumbe wake, alioutoa kwa ajili ya Siku ya Kuombea Amani duniani hapo tarehe Mosi Januari , ambao kwa mwaka huu umeongozwa na Madambiu : Hakuna Mtumwa, sote ni ndugu. Mada iliyofungamana katika moyo wa Papa Francisko, ambaye ameonyesha hamu yake katika kila hali, kiloa mtu auanze mwaka mpya na matumaini mapya sehemu zote duniani, kw akuwa na umoja na muungano kamili uliosimikwa katika moyo wa kuheshimiana, haki na upendo.

Papa anakemea kila aina ya unyonyaji katika maisha yote ya kaijamii akisema , ni unyonyaji ni maovu y yanayo dharirisha mahusiano ya kijamii. Kila mtu wa kila jamii, anayo njaa na kiu kwa ajili ya amani, hivyo ni muhimu tena ni dharura, kujenga amani. Fanyeni amani kila mahali. Katika mzizi wa amani kuna sala, Ni wito wa Papa hasa Wakristo kutenda ipasavyo. Ni lazima kuiomba zawadi hii. Ni lazima kila siku kudhamiria hili.

Alfajiri ya mwaka huu mpya, sisi wote tumeitwa kufufua mapigo ya moyo katika matumaini. Lakini hatuwezi kutenda vizuri katika hili , iwapo hakuna amani tangu nyumbani kwako na katika jamii yako, kazini, safari, na pengine pote ni kufanya amani! Papa anasema hii ni ishara ndogo lakini ya thamani sana. Inaweza kuwagawia wengine mbegu hii ya amani, mbegu ya matumaini, yenye kufungua barabara ya matarajio ya amani.








All the contents on this site are copyrighted ©.