2014-12-29 11:14:38

Agca aweka shada la maua kwenye Kaburi la Yohane Paulo II, miaka 30 baada ya kukutana gerezani!


Mehemet Ali agca, kutoka Uturuki aliyempiga risasi Baba Mtakatifu Yohane Paulo II kunako mwaka 1981, Jumamosi tarehe 27 Desemba 2014 alikwenda kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican ili kutoa heshima zake kwa Mtakatifu Yohane Paulo II na akafanikiwa kuweka shada la maua. Ali Agca alisamehewa na Baba Mtakatifu Yohane Paulo II alipomtembelea gerezani na baadaye Rais Carlo Azeglio Ciampi akamsamehe na hatimaye, kuruhusiwa kutoka nchini Italia kunako mwaka 2000.

Tukio la Ali Agca kutembelea na kuweka shada la maua kwenye Kaburi la Mtakatifu Yohane Paulo II limekwenda sanjari na kumbu kumbu ya miaka thelathini na moja, tangu Baba Mtakatifu Yohane Paulo II alipomtembelea Agca kwenye gereza la Rebbibia, kunako Desemba 1983. Ali Agca aliingia Kanisani kwa uhuru kamili kwani hakuna kizuizi chochote kutoka Vatican anasema Padre Ciro Benedettin, Msemaji msaidizi wa Vatican.

Ali Agca baadaye alikamatwa na Askari wa Italia ili kuhojiwa ikiwa kama alikuwa na nyaraka zilizomwezesha kuingia nchini Italia, lakini kwa bahati mbaya hakuwa wala kibali cha kuingia nchini Italia, hivyo Jeshi la Polisi nchini Italia, limemfukuza nchini humu. Ali Agca kwa mara mbili mfululizo ameomba kukutana ili kuzungumza na Baba Mtakatifu Francisko, lakini hajawahi kupata kibali, Padre Lombardi anasema, shada la maua kwenye Kaburi la Mtakatifu Yohane Paulo II linatosha!







All the contents on this site are copyrighted ©.