2014-12-24 15:12:24

Asanteni sana endeleeni kuvumilia - Papa


Baba Mtakatifu Francisko , Jumanne wiki hii, amepeleka barua ya matashi mema ya Siku Kuu ya Noeli kwa Wakristo wa Mashariki ya Kati, akionyesha ukaribu wake katika wakati huu, ambamo Wakristo wanahangaishwa na ukatili na ghasia za zinazoendelea katika mkoa huo, hasa ghasia zinazojirudia mara kwa mara, zinazofanywa na makundi ya kigaidi.

Papa ameonyesha kuungana na Wakristo hao katika mateso yao na shida zao kutokana na ukosefu wa amani. Amesema, yeye kila siku , hufuatilia taarifa mpya za mateso makubwa yanayo jirudiarudia kwa watu wengi katika Mashariki ya Kati. Na hasa kwa namna ya kipekee kwa watoto, akina mama vijana, wazee, na wakimbizi wote, na wale wote wanaokabiliwa na njaa na kukabiliana na uwepo wa baridi kubwa , bila makazi.

Papa ameandika , katika hali hii ya mateso ya watu hao, ni vigumu kwake kukaa kimya wakati sehemu ya mwili wa Kristo inaumizwa na ukatili wa binadamu. Hivyo anamlilia Mungu, kupitia dhamira na sala zake, Mungu awezeshe uwepo wa juhudi thabiti za kusaidia kwa njia yoyote, ili amani irejee tena kwa wote, na pia ameonyesha ukaribu wake binafsi na mshikamano, kama vile ilivyo kwa Kanisa zima la Ulimwengu kwa kuwapa neno la faraja na matumaini.

Papa kwa namna ya pekee, ametoa salaam na heshima zake kwa viongozi wa Kanisa wote, Mapatriaki, Maaskofu, Mapadre, Watawa wanaume na wanawake, ambao wanaongoza jamii ya Kanisa Mashariki ya Kati , kwa upendo na kujitolea sadaka, licha ya hali hizo za wasiwasi na mateso makubwa. Papa ametaja thamani ya uwepo wao , na kazi ya wale ambao wameweka maisha yao wakfu kwa ajili ya Bwana, kumtumikia kupitia ndugu zao na dada zao , hasa wahitaji zaidi katika yote mawili kiroho na kimwili pia, na hivyo, unakuwa ni ushuhuda wa upendo wake usio kifani! Papa ametaja jinsi uwepo wao ulivyo muhimu katikati ya makundi yao, hasa katika nyakati za shida!
Aidha amewakumbuka vijana akisema anawakumbatia kwa upendo wa kibaba. Amewataka wawe aminifu katika wito wao , na maendeleo yako ya kibinadamu na Wakristo, na kufikia matumaini na ndoto zao. Na pia ametoa heshima zake kwa wazee akisema kumbukumbu zao ni heshima kubwa kwa taifa lao.

Papa ameendelea kuwatia moyo Wakristo wa Mashariki ya kati kwamba, uwepo wao una thamani kubwa katika kumshudia Yesu daima, licha ya matatizo yanayowakabili. Uwepo wao una thamani kubwa kwa ajili ya Mashariki ya Kati. Pamoja na uchache wao , lakini wana wajibu mkubwa katika nchi hii ambamo Ukristo ulizaliwa na kuenea kwingine kote. Wao ni kama chachu dogo. Na pia amewashukuru kwa michango yao mingi ambayo Kanisa hutoa katika maeneo ya elimu, afya na huduma za jamii, kwa ajili ya manufaa ya watu wote wa Mashariki ya Kati , chanzo cha utajiri wa amani katika mkoa huo. Uwepo wa Wakristo hao ni uwepo wake pia . Na amewashukuru kwa uvumilivu wao.
Papa aliendelea kuhimiza waendelee kushirikiana na watu wa dini nyingine,Wayahudi na Waislamu, kama ishara nyingine ya Ufalme wa Mungu, licha ya ugumu uliopo, lakini mwingiliano na majadiliano ni muhimu. Hakuna njia nyingine ya kuwa na maelewano. Mjadala, msingi katika mtazamo wa uwazi, katika ukweli na upendo, pia ni njia bora ya majaribu ya imani kali za kidini, ambayo ni tishio kwa wafuasi wa dini zote. akati huo huo, mazungumzo yalenge katika huduma ya haki na umuhimu wa amani, jambo linalofaa kukumbatiwa na wote.









All the contents on this site are copyrighted ©.