Ugonjwa wa Ebola bado ni tishio kwa maisha na maendeleo ya watu!
Ugonjwa wa Ebola ni kati ya majanga ambayo yametishia usalama na maisha ya watu wengi
Afrika Maghariki katika kipindi cha Mwaka 2014 kiasi cha madaktari waliojisadaka maisha
yao kupambana na ugonjwa huu kutajwa na Jarida la TIMES kuwa ni kati ya watu mashuhuri
kwa Mwaka 2014. Wanachama wa Baraza la Makanisa Ulimwengu wamekuwa mstari wa mbele
katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ebola huko Afrika Magharibi, kiasi cha kuunda
kikosi kazi cha kufuatilia mapambano haya katika ngazi ya kimataifa.
Viongozi
wakuu wa Makanisa wanasema kwamba, ugonjwa wa Ebola umeacha madhara makubwa sana katika
maisha ya watu, kiasi hata cha kukwamisha mchakato wa maendeleo endelevu, mahusiano
na mfungamano wa watu kimataifa. Baraza la Makanisa Ulimwenguni limeendelea kushirikiana
na wadau mbali mbali ili kutoa huduma ya afya kwa wananchi wanaoishi vijijini katika
zile nchi ambazo zimeathirika vibaya kwa ugonjwa wa Ebola.
Ili kufanikisha
mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ebola, kuna haja kwa Jumuiya ya Kimataifa pamoja na
wadau mbali mbali kutambua na kuthamini mila na desturi za Kiafrika kuhusiana na zawadi
ya uhai, ili kuwasaidia wananchi waliokumbwa na ugonjwa huu kuweza kufuata protokali
zinazotakiwa katika kudhibiti kuenea kwa ugonjwa wa Ebola, vinginevyo, Jumuiya ya
Kimataifa inaweza kujikuta kwamba, mikakati na malengo yake hayafanikiwa kwa kama
ilivyopangwa.
Umoja wa Mataifa umedhamiria kufanya kazi kwa kushirikiana na
Makanisa Ulimwenguni, ili kutokomeza ugonjwa wa Ebola ambao bado ni tishio kubwa kwa
maisha na maendeleo ya watu!