(Vatican Radio) Mahujaji na wageni wanaotembelea uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu
Petro katika siku hizi za mwisho za kipindi na Majilio, wanafurahia pia, pambo la
Mti mkubwa wa Krismasi, uliopambwa kwa taa nyingi za kuvutia, ambao taa zake ziliwashwa
rasmi Ijumaa iliyopita 19 ya Desemba.
Kwa miaka mingi ya nyuma Vatican , hapakuwa
na utamaduni wa kuweka mti wa Krismasi katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro.
Lakini mwaka 1982 Papa Yohana Paulo II, alirudisha utamaduni huu wa kupamba uwanja
wa Kanisa Kuu kwa mti mkubwa wa Krismasi kama ilivyokuwa utamaduni Poland, Tangu
wakati huo, nchi nyingi tofauti na mikoa ya Ulaya wamekuwa wakijitolea kwa zamu
kufanikisha uwepo wa pambo hili la mti wa Noel , katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu
Petro .
Mti ya mwaka huu, ambayo ni mti wenye umri wa miaka 70, umetoka katika
Mkoa wa Kusini mwa Calabria, ambkyo Papa Francisco, alitembelea eneo hilo Juni mwaka
huu. Katika waraka wake "Mwanga wa imaniā Papa Francisco, alitumia mfano wa matawi
ya mti, kama jinsi imani kwa Mungu inavyoenea Taa ulimwenguni.
Mti huu wa Krismasi
una urefu wa mita 25.5 kwenda juu na uzito wa tani 8, ni mti wa kuvutia kwa jinsi
hata kwa jinsi shina linavyoonekana , ni shina pacha, mashina mawili tofauti yameungana
pamoja na kuunda mti moja . Shina hili linatumika kama mfano kwamba, hata mwanadamu,
kamwe hawezi kufanya hija ya maisha peke yake, maisha bora daima ni kuungana na
Bwana. Na pambo la pango la Noel, linatazamiwa kusaidia kutoa picha halisi na maana
ya tukio zima la kuzaliwa kwa mkombozi wa dunia katika maisha ya kawaida ya kijamii
.