Mheshimiwa Philip Marmo, Balozi wa Tanzania mjini Vatican katika mahojiano maalum
na Radio Vatican anaelezea kwa ufupi historia na uzoefu wake katika taaluma ya kutunga
sheria za Bunge, Miaka 25 ya Ubunge pamoja na changamoto alizokabiliana nazo katika
uwanja wa kisiasa nchini Tanzania.
Itakumbukwa
kwamba, Balozi Marmo amewasilisha hati zake za utambulisho kwa Baba Mtakatifu Francisko,
hivi karibuni mjini Vatican pamoja na kupata nafasi ya kuonana na kuzungumza na viongozi
mbali mbali wa Vatican, tayari kuanza kutekeleza dhamana na wajibu wake kama Balozi
wa Tanzania mjini Vatican.
Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S. Idhaa ya
Kiswahili ya Radio Vatican.