Tume ya kipapa ya kulinda watoto wadogo yakamilika!
Padre Federico Lombardi, Msemaji mkuu wa Vatican anabainisha kwamba, Baba Mtakatifu
Francisko amekamilisha mchakato wa kuunda Tume ya Kipapa ya kulinda Watoto Wadogo
yenye wajumbe 17 kutoka sehemu mbali mbali za dunia na tayari inaweza kuanza utume
waka kama kawaida. Hawa ni wajumbe wenye ujuzi na taaluma: Saikolojia, afya ya akili,
taalimungu, sheria za Kanisa, ualimu na tafiti za kijamii.
Kuna wanawake nane
na kati yao kuna watawa wa kike wawili; wanaume ni tisa na kati yao kuna Mapadre watano.
Wengine ni waathirika wa vitendo vya nyanyaso za kijinsia ambao kwa sasa wako mstari
wa mbele ili kutoa majibu muafaka. Ifuatayo ni orodha ya wajumbe wa Tume hii ya Kipapa.
Tume hii ina dhamana, weledi na taaluma katika mapambano dhidi ya nyanyaso za kijinsia
kwa watoto wadogo. Hiki ni kielelezo makini kwamba, Kanisa linapania kuwa mstari wa
mbele katika kuwalinda watoto dhidi ya nyanyaso ambalo kwa sasa linaonekana kuwa ni
kati ya matatizo na changamoto kubwa za kijamii.
1. Kardinali Seán O'MALLEY,
OFM Cap., Rais 2. Mons. Robert OLIVER (USA), Katibu mkuu 3. Rev. Luis Manuel
ALI HERRERA (Colombia) 4. Dr. Catherine BONNET (Ufaransa) 5. Marie COLLINS
(Ireland) 6. Dr. Gabriel DY-LIACCO (Ufilippini) 7. Prof. Sheila the Baroness
HOLLINS (Uingereza) 8. Bill KILGALLON (New Zealand) 9. Sr. Kayula Gertrude
LESA, RSC (Zambia) 10. Sr. Hermenegild MAKORO, CPS (Afrika ya Kusini) 11. Kathleen
McCORMACK AM (Australia) 12. Dr. Claudio PAPALE (Italia) 13. Peter SAUNDERS
(Uingereza) 14. Mh. Hanna SUCHOCKA (Poland) 15. Dr. Krysten WINTER-GREEN (USA) 16.
Rev. Dr. Humberto Miguel YÁÑEZ, SJ (Argentina) 17. Rev. Dr. Hans ZOLLNER, SJ (Ujerumani)
Mkutano
wa Tume hii ya Kipapa utafanyika mjini Vatican kuanzia tarehe 6 - 8 Februari 2015
kama ilivyokuwa imepangwa tangu awali.