Jubilee ya miaka 50 iwe ni changamoto ya kusonga mbele kwa imani na matumaini zaidi!
Shirika la Masista wa Kazi za Roho Mtakatifu linaadhimisha Jubilee ya Miaka 50 tangu
lilipoanzishwa wakati huu ambapo Mama Kanisa anaadhimisha pia Mwaka wa Watawa Duniani.
Askofu Isaac Amani Massawe wa Jimbo Katoliki Moshi, Jumatatu tarehe15 Desemba 2014
ameongoza Ibada ya Misa Takatifu kama sehemu ya kilele cha Maadhimisho ya Jubilee
ya Miaka 50 tangu Shirika hili lilipoanzishwa nchini Tanzania.
Askofu Joseph
Mlola wa Jimbo Katoliki Kigoma anawaalika Masista hawa kufanya tafakari ya kina, ili
miaka 50 iliyopita iwe ni fursa ya kumtolea Mwenyezi Mungu shukrani kwa wema na ukarimu
wake katika maisha na utume wao kwa Watu wa Mungu Afrika Mashariki.
Jubilee
hii anasema Askofu Mlola, iwe ni nafasi ya kuangalia maendeleo na changamoto wanazokabiliana
nazo, huku wakidhamiria kuyapyaisha maisha na utume wao kwa Familia ya Mungu, kwanza
kabisa kwa kubainisha utambulisho wao kama Wanashirika ili kujenga na kuimarisha umoja
na mshikamano, kama kielelezo makini cha ushuhuda makini wa maisha ya kitawa.
Askofu
Joseph Mlola anawaombea Masista hawa neema na baraka kutoka kwa Roho Mtakatifu, ili
azidi kuwaongoza, kuwaimarisha na kuwategemeza zaidi, ili waweze kusonga mbele kwa
imani na matumaini pasi na kukata na tamaa kwa changamoto na magumu mbali mbali wanayokutana
nayo!
Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S. Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.